WANUFAIKA WA TASAF KULIPWA 261,835,350 JIJINI DODOMA

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma kuanza kulipa shilingi 261,835,350 wanufaika 8,017 wa mpango wa kunusuru kaya masikni katika dirisha la Septemba-Oktoba, 2022.

Sekunda Kasese


Kauli hiyo ilitolewa na Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Sekunda Kasese alipokuwa akiongelea utaratibu wa kulipa wanufaika wa TASAF katika dirisha hili ofisini kwake.

Kasese alisema “katika kipindi cha malipo ya dirisha la mwezi Septemba hadi Oktoba, 2022 tumepokea shilingi 261,835,350 kwa ajili ya walengwa 8,017 waliopo katika mitaa 222 ya Jiji la Dodoma. Tuna walengwa 222 wanaolipwa kwa njia ya wakala (OTC) na wakala wa mitandao ya simu. Tuna walengwa 741 wanaolipwa kwa njia ya mitandao kwa kutumiwa fedha moja kwa moja kwenye simu. Kuna utaratibu maalum wa kuweza kuwafanya walengwa wanaaopokea fedha kwa njia ya mitandao na OTC kuna fomu watakazopelekewa ili wasaini kuthibitisha malipo waliyopokea”.

Katika dirisha hilo, wamepokea kiasi cha shilingi 100,000 sawa na asilimia 1.5 ya mtaa. “Fedha hii inatumika kulipa wenyeviti wa mitaa, watendaji na wajumbe wa serikali za mitaa na fedha inayobaki inatumika kwa shughuli za maboresho ya ofisi na shughuli kama kutoa copy na nauli” alisema Kasese.

Mratibu wa TASAF alisema kuwa katika dirisha hili wajumbe wa kamati za mpango za jamii (CMC) wamerejeshwa. “CMC wamerejeshwa na kazi zao ni kushughulikia masuala mbalimbali ya walengwa katika mitaa yao. Na wataanza kufanya kazi katika dirisha hili kulingana na miongozo ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini” alisema Kasese.

Akiongelea maboresho ya warsha za jamii, alisema kuwa kila dirisha la malipo limekuwa na mada tofauti. “Katika kipindi hiki cha pili cha awamu ya tatu ya TASAF, wameleta mwongozo ulioboreshwa wa warsha za jamii (community sessions) malipo ya mwezi Mei-Juni, tulifanya mada ya kwanza ambayo ni uhawilishaji fedha. Malipo ya Julai-Agosti tulifanya mada ya miradi ya kutoa ajira za muda na malipo ya mwezi Septemba-Oktoba tutafanya mada ya uwekaji wa akiba na uchumi wa kaya. Mada hizi zinafundishwa nchi nzima” alisema Kasese.

Aidha, alimshukuru Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kuhakikisha fedha hizo zinawafikia walengwa kwa wakati.

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.