WAZIRI KALEMANI ATOA BEI ELEKEZI KUUNGANISHA UMEME WAKAZI WA JIJI LA DODOMA

Na. Kadala Komba, Dodoma

WAZIRI wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani ametoa bei elekezi ya sh. 27,000 kwa wananchi wote wa Jiji la Dodoma wanaohitaji kuunganishiwa umeme majumbani kuwawezesha wananchi wote kupata huduma ya umeme kwa urahisi.

Waziri Dkt. Medard Kalemani


Waziri Dkt. Kalemani ametoa bei elekezi hiyo jana mara baada ya kufanya ziara katika kata ya Ntyuka jijini, Dodoma kwa lengo la kukagua maendeleo ya miradi mitatu ya umeme ikiwemo, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Alisema kufuatia ziara hiyo alibaini wananchi wengi wa eneo hilo hawajapata huduma hiyo kutokana na bei walizokuwa wakitozwa ambao husababisha kushindwa kumudu na ta kukwamisha nia ya serikali ya kufikisha umeme kwa wananchi.

“Tuna mradi na TANESCO wanaendea na zoezi la kuwapitishia umeme wananchi huu una gharama takribani bilioni 12 zinakuja Dodoma ndani ya miezi sita lakini mradi wa pili wa Desification amabo wakandarasi wameshaanza bilioni 48 zinaingia Dodoma tuna uhakika hakuna mwana Dodoma atakayeachwa,” alisema.

Aidha, Waziri Dkt. Kalemani ameelekeza wakandarasi  kuhakikisha wanasambaza umeme kwenye maeneo yote waliyo elekezwa  kabla ya siki 14 na kuhakikisha hawaruki nyumba yOyote   kwani lengo la serikali ni kuhakikisha wananchi wote wanapata  huduma  hiyo  ndani ya miezi 12.

“Kukatika kwa umeme mtoe taarifa ndugu zangu ni wapi umekatika mimi naletewa taarifa nashindwa kumtuma Meneja aende wapi matokeo yake unakaa na tatizo mwezi mzima na niagize TANESCO muweke madawati ya huduma kwa wateja walio mbali na huduma za tanesco umbali wa zaidi ya kilometa 60 haiwezekani mwananzengo asafiri kilometa 200 kufuta umeme kwa kulipa sh.27,000,” alieleza Dkt. Kalemani.

Akizungumza katika ziara hiyo Mbunge wa Dodoma mjini, Anthony Mavunde ameishukuru serikali kwa namna ambavyo imeendelea kutatua changamoto za masuala ya umeme pamoja na kutoa bei elekezi ambayo itakuwa rafiki kwa wananchi wote.

Mbunge Anthony Mavunde


“Niishukuru sana Serikali yetu kwa kuendelea kutatua kero zanishati kwa wananchi wake. Mheshimiwa Waziri leo tumetumia Ntyuka kama kielelezo cha maeneo mengine mengi ya jiji la Dodoma,” alibainisha.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Bwawani, Abel Majengo  amemshukuru waziri kufika katika eneo hilo na kutoa maelekezo ambayo yatawasaidia Wananchi Kupata umeme kwa haraka.

“Kama ulivyotoa maelekezo serikali inafanya klazi na sasa tutawaambia wananchi tangu miaka yote kulikuwa hakijaguswa na mradi wa umeme bei ilikuwa ni chagamoto watu wengi wamefanya wiring kwa sababu umetoa maelekezo tutaelekea tu kwenye maelekezo hayo,” alieleza.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.