Na. OMM Rukwa
Mkuu
wa Mkoa Rukwa Queen Sendiga ameagiza Wakurugenzi wa Mamlaka za serikali za
mitaa kuchukua hatua za kuwarejesha watendaji na watumishi wa serikali wanaotuhumiwa
kuharibu miradi ya wananchi ili wajibu tuhuma zao.
Kauli
hiyo ameitoa jana (Jumatatu, Novemba 07, 2022) wakati akizungumza kwenye
mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Kabwe wilaya ya Nkasi ambapo
walilalamika kuwa Mtendaji amehamishwa baada ya kuharibu mradi wa zahanati.
Mkuu
wa Mkoa huyo alitembelea zahanati ya kijiji cha Kabwe na kujionea hali ya
kukwama kwa ujenzi wa jengo la mama na mtoto ambalo linadaiwa kupatiwa vifaa
vya mabati na saruji toka kwa wafadhili mwaka 202o lakini halijakamilika.
“Mtendaji
wa Kata aliyekuwa hapa arejeshwe kuja kutoa majawabu ya tuhuma za kutokamilika
zahanati ya kijiji cha Kabwe wakati vifaa vya ujenzi vilitolewa na wafadhili”
alisema Sendiga.
Katika
hatua nyingine Sendiga ameagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) kuchunguza mradi wa ujenzi wa zahanati hiyo na kwa wahusika
watakaobainika hatua za kisheria zichukuliwe haraka.
Kwa
upande wake Diwani Kata ya Kabwe Asante Lubisa alikiri kupokelewa kwa vifaa vya
ujenzi wa zahanati hiyo toka Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) mwaka 2020
lakini kutokana na ramani iliyopangwa kubadilika mradi umeshindwa kukamilika
hadi sasa.
Mkuu
wa Mkoa huyo akiwa wilayani ya Nkasi alikagua kituo cha Afya Kasu, Hospitali ya
Wilaya, ujenzi wa madarasa sekondari ya Kabwe na bandari ya Kabwe ambapo
alisema hatokubali kuona miradi ikisua sua.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga akikagua bandari ya Kabwe jana alipotembea kuona utendaji kazi wake
Mwisho.
Comments
Post a Comment