TAKUKURU DODOMA: TUMEANZISHA UFUATILIAJI WA ZOEZI LA UGAWAJI WA PEMBEJEO ZA KILIMO ILI KUZUIA UDANGANYIFU

 


Dodoma.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoa wa Dodoma imeanzisha ufutialiaji wa zoezi la ugawaji wa pembejeo za kilimo ili kuzuia vitendo vya udanganyifu na ubadhirifu vilivyokuwa vikifanywa na baadhi ya watendaji na mawakala wa pembejeo.

Akiongea mkoani hapa  Novemba 29,2022 Mkuu wa Taasisi hiyo Sosthenes Kibwengo amesema huko nyuma zoezi hilo lilikuwa likikabiliwa na changamoto hizo hali iliyopelekea baadhi ya watendaji hao kufunguliwa mashauri ya jinai mahakamani kutokana na vitendo hivyo.

‘Tunawasihi wahusika wote katika mchakato huo kuzingatia taratibu kwani hatua kali zitachukuliwa dhidi ya wote watakaobainika kufuja pembejeo .’’ amesema

Aidha, Kibwengo amesema wamekuwa wakishirikiana na halmashauri za mkoa wa Dodoma kuhakikisha ushuru na tozo zingine zinazokusanywa kwa njia za mashine za Kieletroniki za POS zinawasilishwa benki kwa wakati.

‘’Ufuatiliaji huu umewezesha kuokoa fedha shilingi 75,524,700 zilizobaki mikononi mwa mawakala kwa muda mrefu kuwasilishwa benki.’’ ameongeza 

Kuhusu chambuzi 10 za mifumo ya utendaji na utoaji huduma ili kubaini mianya ya rushwa , amesema wamebaini mfumo wa malipo ya fedha taslimu katika halmashauri ya wilaya ya Bahi taratibu za matumizi ya fedha taslimu zinakiukwa kwa fedha kutolewa benki na kuhifadhiwa muda mrefu bila kutumika.

‘’Na hivyo kutengeneza mwanya wa ubadhirifu wa fedha hizo. Yamebainika matumizi kinyume na makusudio ,fedha kutolewa benki ili kufanya kazi ambazo tayari fedha zake zilishatolewa awali na malipo kufanyika bila kuonyesha sababu uhalali wa malipo hayo.’’ amesema

Katika hatua nyingine Kibwengo amezungumzia kuhusu vitendo vya rushwa ya ngono vinavyo fanyika katika maeneo mbalimbali nchini kuwa ni muhimu kuvunja ukinya dhidi ya vitendo hvyo.

‘’Rushwa ya ngono ni tatizo linaloingia mpaka kwenye utu wa mtu. Tuvunje ukimya tuachane na hii tabia yetu ya kuogopa kusema  haya mambo. Haya mambo si ya kificho kiivyo kwa sababu yanakuathiri wewe.’’

Hatahivyo, amesema wanatarajia kuweka nguvu katika kuelimisha wananchi ili waweze kushiriki kikamilifu  katika  kuzuia  vitendo vya rushwa .

Mwisho. 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.