Na
Mwandishi wetu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe.
George Simbachawene amepongeza Tume ya kudhibiti UKIMWI, Wizara ya Afya na
Wizara ya TAMISEMI katika Mkakati wa kupambana na Ukimwi kama janga la kitaifa.
Hayo yamesemwa Waziri na Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na
Uratibu Mhe. George Simbachawene Jijini Dar es saalam, wakati wa uzinduzi wa
taarifa ya hali ya UKIMWI duniani yenye Kauli Mbiu inayosema Dangerous
Inequalities iliyotolewa Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia Ukimwi Duniani
UNAIDS Bi, Winnie Byanyima.
“Serikali imedhamiria kuweka usawa wa kijografia usawa
kimazingira usawa kati ya watoto na wakubwa na usawa wa kiuchumi ili
kuhakikisha watu wote wanapata huduma sawa ili wasiathirike na wale walio
athirika wapate huduma za matibabu lakini pia huduma sawasawa kuhakikisha
wanaendesha maisha yao.”
Akitoa taarifa hiyo Mkurugenzi Mtendaji anayeshughulikia Ukimwi
Duniani UNAIDS Bi, Winnie Byanyima amesema Tanzania imejitahidi kupunguza
Ongezeko la Maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI kila Mwaka kwa miaka kumi
mfululizo.
“Tanzania Imejitahidi kupunguza vifo vinavyosababishwa na UKIMWI
na imekuwa ikifanya vizuri katika mapambano dhidi ya virusi vya UKIMWI.”
Comments
Post a Comment