SERIKALI: LENGO LETU NI KUJENGA MAZINGIRA BORA YA UFANYAJI BIASHARA KWENYE SEKTA YA MIFUGO


DODOMA.


Wizara ya Mifugo na Uvuvi imekutana na wadau mbalimbali ikiwamo wadau wa mifugo kwaajili ya kujadiliana na kuwasilisha changamoto za kikodi pamoja na mapendekezo ya kuboresha mazingira ya kibiashara yatakayo jadiliwa kwenye Bunge lijalo la Bajeti 2023/2024.

Akiongea katika kikao kilicho wakutanisha wadau hao jana jijini Dodoma Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Sekta ya Mifugo Tixon Nzunda amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wanajenga mazingira bora ya ufanyaji biashara na uwekezaji kwenye Sekta hiyo

‘’Tunajielekeza kufanya mabadiliko makubwa kuwezesha sekta kuweza kubadilika. Moja ambalo ndio kubwa ni tija ili kusukuma sekta kufanya kazi zake kitaalam kwa maana yakwamba hatuwezi kuzungumza tija kama hakuna utaalam.’’ amesema Nzunda 

Aidha, amesema mwelekeo wao ni kuifanya sekta hiyo inafanya kazi kibiashara ili kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa hapa nchini zinakidhi viwango vya kitaifa na kimataifa kwaajili ya kupata soko.

‘’Tusaidiane na wenzetu kuhakiksha masoko yanapatikana ya ndani na nje.  Ili kuweza kuongeza wigo wa kukua kwa sekta yetu. Na katika hilo Serikali kwa mwaka huu wa fedha imejithidi kuwekeza katika maeneo haya hasa kwa sekta ya nyama.'' ameongeza 

Katika hatua nyingine amesema wamejipanga kuimarisha huduma za utafiti ili  kusukuma kazi zinazofanywa na wadau ziweze kufanywa kutokana na utafiti uliofanyika.

''Ndio maana tumejikita kuimarisha taaasisi ya TARIRI iweze kufanya kazi yake Kupata mbegu bora.  Hapa kuna changamoto nyingi tunajikita zaidi kuhakikisha tunapata mbegu bora za malisho.'' amesema 

Mwisho. 



Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.