SERIKALI KUBORESHA HUDUMA ZA KIBINGWA MKOANI IRINGA

Na WAF- DOM

 

SERIKALI Kupitia Wizara ya afya inaelekea kukidhi kiu ya Wananchi wa Mkoa wa Iringa kwa kupeleka kusoma jumla ya madaktari 12 watakaotoa huduma katika fani mbalimbali katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

 

Mhe. Dkt. Godwin Mollel

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya Mhe. Dkt. Godwin Mollel leo Novemba 8, 2021 katika kikao cha bunge, Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mhe. Nancy Hassan Nyalusi Mbunge wa viti maalumu. 

 

Amesema, Katika kuongeza idadi ya madaktari bingwa, Wizara imepeleka kusoma jumla ya madaktari kumi na mbili (12) kutoka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Iringa ambao watasaidia kuboresha huduma kwa wananchi wa Mkoa huo.

 

Akifafanua hilo Dkt. Mollel amesema, madaktari hao ni pamoja na; madaktari wawili wanasomea kinywa, sikio na koo, madaktari bingwa wa mifupa wawili, daktari wa magonjwa ya dharura mmoja, madaktari bingwa wa Watoto wawili, madaktari bingwa wa magonjwa ya ndani wawili, daktari bingwa wa meno mmoja, daktari bingwa wa usingizi mmoja na daktari bingwa mbobezi wa masuala ya Watoto mmoja. 

 

Aidha, Dkt. Mollel amesema, hadi sasa Hospitali hiyo ina jumla ya madaktari bingwa kumi na moja 11, madaktari bingwa wa afya ya akina mama na uzazi wanne, madaktari bingwa wa upasuaji wawili, daktari bingwa wa magonjwa ya ndani mmoja, daktari bingwa wa Watoto wawili, daktari  bingwa wa macho mmoja  na daktari bingwa wa mionzi mmoja.

 

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.