SERIKALI KUANZA MCHAKATO WA KUHAKIKI STAHIKI ZA WATUMISHI WALIOONDOLEWA KAZINI VYETI FEKI

Na. Rhoda Simba, Dodoma

 

SERIKALI imeaanza mchakato wakuhakiki stahiki za watumishi walioondolewa kazini kwa kosa la kughushi vyeti kama ilivyoelekezwa na Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, siku ya Mei Mosi 2022.

 

CPA. Hosea Kashimba

Akitoa ufafanuzi wa kile kilichofikiwa katika ulipaji wa stahiki hizo Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa watumishi wa Umma CPA. Hosea Kashimba alisema mfuko huo unatarajia kulipa watumishi hao elfu tisini 9,000 ambao watatumia takribani shilingi Bilioni 20.

 

"Mchakato umeanza tarehe 1 Novemba kama ilivoagizwa na Rais na sisi tayari tumeanza kupokea nyaraka kutoka kwa waliokuwa waajili wa wafanyakazi hao, na tutakapo jiridhisha tutalipa fedha hizo kwa wale wote wanaostahiki.

 

Na kuhusu watumishi walifatiki na wanapaswa kurejeshewa michango yao wale walioandikwa kwenye urithi wafanye utaratibu wa kupata fedha hizo kwa kufika katika Ofisi walizokuwa wameajili watumishi waliofariki ili waweze kupatiwa utaratibu wa namna ya kuapata fedha hizo," alisema.

 

Aidha, alieleza kuwa wakati wa kuunganishwa mifuko kiasi kilichokuwa kinalipwa kama pensheni kwa mwezi kwa wastaafu kilikuwa ni shilingi bilioni 34 lakini mpaka kufikia sasa wastani wa kiasi cha shilingi bilioni 60 kinalipwa bila kukosa kwa wastaafu zaidi za 150,000 Kila ifikapo tarehe 25 Kila mwezi.

 

Alisema mifuko hufanya uwekezaji katika maeneo mbalimbali ikiwemo uwekezaji kwenye miradi ya serikali,wakati wa kuunganishwa mifuko PSSSF ilirithi madeni ya serikali yaliyohakikiwa yenye thamani ya shilingi  bilioni 731.40 mpaka sasa kiasi cha shilingi bilioni 500 kimelipwa na Serikali.

 

"Pia nirudie kuishukuru Serikali ya awamu ya 6 kwa kutambua deni la michango kabla ya 1999 maarufu kama (pre 99 liability) ambalo ni shilingi Trilioni 4.60 kwa kutoa hati fungani maalum yenye thamani ya shilingi Trilioni 2.17, haya yote yanaleta matumaini ya kuwa na Mfuko wenye ustahimikivu na endelevu kwa ustawi wa wanachama," alisema.

 

MATARAJIO YA BAADAE

 

Ni pamoja na kuongeza vituo vya uhakiki katika Halmashauri mbalimbali na kuanzisha utaratibu wa kujihakiki kwa simu janja, Kila taarifa ya wanachama iwe kwenye mfumo, usimamizi Bora wa miradi ili kupata matarajio kusidiwa.

 

Na kuhakikisha mifumo ya PSSSF inasomana na mifumo mingine kutoka taasisi nyingine za umma ya watoa huduma,kurahisisha uandikishaji wanachama na uletaji wa madai kupitia mtandao (online claim submission), utaratibu huo utasaidia kutoa huduma kwa haraka na kupunguza matumizi ya karatasi, kubuni mifumo mipya na salama ya TEHAMA kulingana na mahitaji ya Mfuko, kutumia mifumo ya tehama asilimia 85 ikiwa malengo ni kutumia asilimia 100 ifikapo 2023, katika shughuli za Mfuko hivyo kuboresha utoaji wa huduma.

 

Pia alisema kuwa Kwa kipindi cha miaka 4 mfululizo Mfuko umekaguliwa na kupata hati safi na kuibuka mahindi wa tuzo inayotolewa na NBAA kwa utunzaji bora wa mahesabu ya mwaka 2019/20 katika sekta ya hifadhi ya jamii na bima.

 

"Mfuko kupitia Idara ya Manunuzi umeendelea kufanya manunuzi Kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2021 ulipata matokeo bora ya asilimia 94 na Mfuko unatambua moja ya changamoto kubwa kwa jamii yetu ni uelewa mdogo kuhusu sekta ya hifadhi ya jamii,

 

PSSSF imejipanga vizuri kuendelea kutoa elimu kwa wanachama na watanzania wote ili kuhakikisha sekta hii inafamika vyema ili kuendelea kutoa mchango katika uchumi wa nchi yetu," alisema.

 

Mfuko wa PSSSF ulianzishwa mwaka 2018 kupitia sheria ya Mfuko wa hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma namba 2 ya mwaka 2018, Mfuko huu ni matokeo ya kuunganishwa kwa iliyokuwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ya GEPF (1942), LAPF (1944), PPF (1978) na PSPF (1999).

 

Mwisho

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.