Na. OMM Rukwa
Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga ameelekeza halmashauri zote mkoani humo kuandaa
maadhimisho ya wiki ya utoaji elimu ya lishe bora katika ngazi za vijiji ili
kukabiliana na tatizo la udumavu.
Ametoa
kauli hiyo leo (Novemba 04, 2022) mjini Sumbawanga wakati wa hafla ya kukabidhi
pikipiki Kumi na Mbili (12) kwa maafisa lishe wa halmashauri zilizotolewa na
serikali kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la udumavu ambao kwa Rukwa upo
asilimia 47.9 kwa takwimu za mwaka 2018.
Sendiga
alibainisha kuwa maadhimisho hayo yakifanyika itakuwa jukwaa zuri la wataalam
wa lishe kutoa elimu ya uandaaji vyakula bora na ulaji sahihi kwa kutumia
vyakula vinavyopatikana kwenye mazingira ya Rukwa kwa kuwa mkoa huo ni
mzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula.
Akitoa
taarifa ya vifaa hivyo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Ibrahim Isaack
alisema jumla ya pikipiki Kumi na Mbili zimetolewa kwa Halmashauri za Kalambo
(4), Sumbawanga Vijijini (3), Nkasi (3) na Manispaa ya Sumbawanga (2).
Dkt.
Ibrahim alisema pikipiki hizo zitakwenda kufanya kazi ya elimu ya lishe,
kuboresha utoaji chanjo na kufuatilia magonjwa ya milipuko vijijini.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga (wa kwanza kushoto) akipata maelezo kuhusu pikipiki (12) zilizotolewa na serikali kwa ajili ya maafisa Lishe kwenye halmashauri za Rukwa leo mjini Sumbawanga. |
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Queen Sendiga akikata utepe wakati wa hafla ya kukabidhi pikipiki (12) kwa maafisa lishe wa halmashauri za Rukwa zitakatumika kutoa elimu ya kudhibiti udumavu vijijini |
Mwisho.
Comments
Post a Comment