Na. Rhoda Simba, Dodoma
KATIKA kuimarisha ufanisi wa utendaji kazi wa wahandisi nchini, Bodi ya Wahandisi
(ERB) imesema imeweka mipango ya kukuza na kuimarisha weledi wa sekta ikiwemo
na kupambana na vitendo vya rushwa.
Msajili wa Bodi ya Wahandisi, Bernad Kavishe
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma wakati akielezea
utekelezaji wa majukumu ya bodi hiyo na vipaumbele vyake kwa mwaka wa fedha
2022/2023 Msajili wa Bodi ya Wahandisi, Bernad
Kavishe amesema Bodi itaweka maslahi ya Umma mbele ikiwemo na kuzingatia
maadili.
"Wahandisi pia lazima wadhibitiwe wawe na nidhamu na maadili mema
wawe na uadilifu na kwa kifupi wahandisi tunaweka maslahi ya Umma mbele na
maslah yetu binafsi nyuma na ndio maana tunachukua kiapo kuapa kuweka maslahi
ya Umma mbele.
"Bodi ipo mstari wa mbele katika kupambana na rushwa manake rushwa
ni adui wa uhai siyo tu adui wa haki lakini malengo mahususi ya bodi ni
kuimarisha na kuhakikisha udhibiti wa kazi za wahandisi na taaluma ya
wahandisi kwasababu uhandisi hauishii shuleni uhandisi ni tunahakikisha mpaka
mtu ana staafu" alisema Mhandisi
Kavishe.
Aidha, Mhandisi
Kavishe alitoa wito
kwa watu wenye miradi kuacha kutumia wahandisi ambao hawajasajiliwa na
bodi hiyo ili kuondokana na malalamiko pale wanapoharibiwa kazi zao.
"Kinyume cha sheria kabisa kupata huduma za kihandisi nje na
watu ambao hawajadhibitishwa na bodi mbalimbali za kitaaluma, ile
leseni tunayokabidhi ile ndio kielelezo ambacho serikali imeipitisha
kwamba huyu mtu kapata elimu sahihi hawana mashaka nae na ujuzi wake upo
hai" alisema Mhandisi
Kavishe.
Nae Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa alisema Serikali
imewekeza fedha nyingi kwenye ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo barabara
majengo na tayari imezalisha wahandisi zaidi ya elfu 33 na endapo miradi
ikiharibiwa ERB inahusika.
"Kuna kazi kubwa inafanyika na miradi mingi ndani ya nchi yetu
ambayo inategemea ushauri wa wahandisi hawa na nichukue nafasi hii
kuwapongeza mpaka sasa nchi yetu imezalisha wahandisi zaidi ya elfu 33 na
26 wapo sokoni wanafanya kazi, ikumbukwe kuwa tulipokuwa tunapata
uhuru mwaka 1961 tulikua na wahandisi wawili tuu leo tunazungumzia hawa walio
kazini na vijana bado wapo vyuoni wanasoma wanaendelea kuzalishwa" alisema Msigwa.
Mwisho
Comments
Post a Comment