Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT Tanzania Musa Masanja Magwesela amesimikwa 6 Novemba, 2022 baada ya kuchaguliwa katika mkutano wa Sinodi kuu ya Kitaifa iliyofanyika mwezi wa tisa mwishoni katika kanisa la AICT Buzuruga Mwanza.
Katika tukio hilo la kuwekwa Wakfu ambalo lilihudhuriwa na Viongozi
mbalimbali kutoka Serikalini na watumishi wa Mungu, pia alisimikwa Askofu Mkuu
Msaidizi ambaye ni Askofu wa Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota.
Tukio la kuwekwa Wakfu kwa Askofu Mkuu na Msaidizi wake lilifanyika katika
kanisa la AICT Makongoro kuanza asubuhi saa 2 hadi saa 8 mchana, lilihudhuriwa
na umati mkubwa wa waumini kutoka madhehebu mbalimbali Mkoani Mwanza na nje.
Akizungumza kwa niaba ya Serikali Mgeni Rasmi wa sherehe hizo Waziri wa
Madini, Dkt. Doto Biteko
alimpongeza Askofu Mwageswela na Msaidizi wake Askofu Bugota kwa kuaminiwa
katika nafasi hizo na kuomba wawaunganishe waumini wa Kanisani hilo ili
liendelee kuongezeka kwa idadi ya watu.
"Baba Askofu Mkuu na Msaidizi wake mmeaminiwa sana, mmepewa nafasi
ya kumtumikia Mungu na kanisa la AICT Tanzania, fanyeni kazi ya kuhubiri Neno
la Mungu kiroho na kimwili ili kanisa hili liwe na maendeleo makubwa"
alisema Waziri Dkt. Biteko.
"Serikali ya Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan iko bega kwa bega
na wewe katika kuwasaidia wananchi wapate kuponywa katika mambo ya kiroho na
kimwili maana kanisa lina nafasi kubwa katika maisha ya mtu"
Dkt. Biteko
alisema anaamini katika uongozi wa Askofu Mkuu Musa Magwesela na Msaidizi wake
Askofu Zakayo Bugota, ndio maana wamepewa miaka mingine kuongoza kanisa hilo
katika muhula wa pili.
Akitoa salama za kanisa baada ya kuwekwa Wakfu Askofu Mkuu Magwesela
alisema wanashukuru sana kupewa nafasi hiyo kumtumikia Mungu na kuomba kupewa
ushirikiano ili waweze kutimiza matarajio ya kanisa. Huku akiomba Serikali
kutatua migogoro iliyopo kwenye umiliki wa viwanja mali ya kanisa ila kuna watu
wanaviingilia kinyemela.
MWISHO
Comments
Post a Comment