UJENZI WA DARASA LUKUNDO SEC UMEFIKIA 30%


Na. Prisca Maduhu, DODOMA

Ujenzi wa darasa katika shule ya sekondari Lukundo umefika asilimia 30 ukiwa katika hatua ya lenta ukilenga kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na pia kuwapokea kidato cha kwanza mwaka 2023.

Hatua ya ujenzi wa darasa na chumba kidogo cha ofisi ya walimu

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa shule ya sekondari Lukundo, Mwl. Asifu Makonda wakati akisimamia mradi wa ujenzi wa darasa moja na ofisi ndogo ya walimu ujenzi unaotekelezwa katika Mtaa wa Mtakuja Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mwl. Makonda alisema kuwa shule hiyo ilipokea kiasi cha shilingi 20,000,000 katika utekelezaji wa mradi huo. Kiasi hicho cha fedha kilipokelewa tarehe 1-10-2022 na kuanza ujenzi rasmi tarehe 11-10-2022. 

Aliendelea kusema kuwa, fedha hizi zitatumika katika ujenzi wa darasa moja, ofisi ndogo ya walimu na ununuzi wa vifaa vya ujenzi.

Mkuu wa shule alisema kwamba mpaka sasa wametumia kiasi cha shilingi 8,000,000 na kubakiwa na shilingi 12,000,000 kwenye akaunti. Ujenzi huo unahatua nane, ukiwa katika hatua ya tatu ya utekelezaji wake kuelekea ufungaji wa lenta, sawa na asilimia 30 ya ujenzi, alielezea.

Alisema kuwa kabla ya kuanza kutekeleza mradi huo aliunda kamati tatu ambazo ni kamati ya ukaguzi na mapokezi, kamati ya ujenzi na kamati ya manunuzi. “Darasa hili moja na ofisi ndogo ya walimu ni msaada mkubwa ambao tunaishukuru Serekali kupitia Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mradi huu. katika shule yetu, itasadia kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kuwapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023 na kwa walimu itasadia kuongeza vyumba vya kujandaa ili kuongeza uwajibikaji,” alisema Mwl. Makonda.

Ikumbukwe kuwa shule ya sekondari Lukundo ilianzishwa mwaka 2007, mpaka sasa inawanafunzi 1,315 ambapo wasichana ni 744 na wavulana ni 571.

 


Mwisho

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.