UJENZI WA DARASA ITEGA SEC KUPUNGUZA MSONGAMANO WA WANAFUNZI

Na. Prisca Maduhu, DODOMA

Shule ya Sekondari Itega inatekeleza mradi wa ujenzi wa darasa na ofisi ndogo ya walimu kwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kuwapokea kidato cha kwanza mwaka 2023 ili kuimarisha ufanisi wa kazi na kupunguza msongamano wa walimu katika ofisi moja.

Hatua ya ujenzi wa darasa na ofisi


Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa shule ya sekondari Itega, Mwl. Briton Bwatota wakati akisimamia mradi wa ujenzi wa darasa moja na ofisi ndogo ya walimu katika shule ya sekondari Itega iliyopo Kata ya Nkuhungu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Mwl. Bwatota alisema kuwa shule ya sekondari ya Itega ilipokea kiasi cha shilingi 20,000,000 katika utekelezaji wa mradi huo. Aliongeza kuwa kiasi hicho cha fedha kilipokelewa tarehe 1-10-2022 na kuanza ujenzi rasmi tarehe 10-10-2022. 

Aliendelea kusema kuwa, fedha hizi zitatumika katika ujenzi wa darasa moja, ofisi ndogo ya walimu, ununuzi wa vifaa vya ujenzi pia ununuzi wa samani za darasani ambazo ni viti na meza.

Mkuu huyo wa shule alisema kwamba kiasi cha shilingi 6,434,000 kimetumika na kubakiwa na shilingi 13,566,000 kwenye akaunti. Ujenzi huo umefikia katika hatua ya kuweka lenta ambapo ni sawa na asilimia 63% ya ujenzi huo, aliongeza.

Alisema kuwa aliunda kamati tano kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa mradi huo. Alizitaja kamati hizo kuwa ni kamati ya mapokezi, kamati ya ujenzi, kamati ya manunuzi, kamati ya utekelezaji mradi na “tender bord”.  Pia alisema kuwa walitoa matangazo ya kutafuta fundi ujenzi, ambapo tangazo hili walilitoa katika ofisi ya kata na kubandika matangazo, na baadae kuwapata mafundi na kuwafanyia usaili ili kumpata fundi ambaye amekidhi vigezo.

“Mradi huu ni msaada mkubwa katika shule yetu, utasadia kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kwa walimu utasadia kuongeza uwajibikaji,” alisema Mwl. Bwatota.

Ikumbukwe kuwa shule ya sekondari Itega ilianzishwa mwaka 2007, mpaka sasa ina wanafunzi 771 ambapo wasichana ni 323 na wavulana ni 448.

 



Mwisho


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.