SERIKALI YABAINISHA UJENZI WA MIRADI YA BARABARA INAYOENDELEA NCHI NZIMA...

 


Na Mwandishi Wetu,Dodoma .

Serikali imesema jumla ya  Miradi 44  ya Barabara yenye kilomita 1,523 inaendelea na ujenzi nchi nzima ikigharimu kiasi shilingi trilioni 3.8 .

Hayo yamesemwa Oktoba 29,2022 na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania TANROADS Mhandisi Rogatus Mativila wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya Wakala huo Kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kupitia vyombo vya habari.

Aidha, amesema miradi hiyo ,ipo katika hatua mbalimbali za ujenzi ambayo inahusisha miradi inayo gharamiwa na Serikali kwa kutumia fedha za ndani na inayogharamiwa Kupitia Washirika mbalimbali mbalimbali wa Maendeleo.

"Mradi mkubwa wa ujenzi wa Kiwanja cha ndege cha Msalato unaojumuisha ujenzi wa njia ya kurukia ndege na majengo ya abiria unaendelea chini ya ufadhili wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) kwa gharama ya Shilingi Bilioni 360." amesema

Pia, amesema Miradi ya barabara 62 iko katika hatua mbalimbali za manunuzi kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

"Miradi ya EPC+ F Wizara ya Ujenzi kupitia TANROADS imeanza utekelezaji wa Miradi ya EPC + F yenye urefu wa kilometa 2,533km. Makampuni yaliyokuwa “shortlisted’ yamealikwa tarehe 22 Septemba, 2022  kuwasilisha zabuni." Ameongeza

Wakati huo huo, amesema jumla ya miradi 43 ya barabara yenye urefu wa kilometa 2,021.04 na gharama ya Shilingi Bilioni 9.6 ipo katika hatua mbali mbali za upembuzi yakinifu na usanifu. 

"Miradi ya Ujenzi wa Barabara na Viwanja vya Ndege ambayo imesainiwa mikataba katika Mwaka wa Fedha 2021/22 (Julai 2021 hadi Mei 2022) Katika mwaka wa fedha 2021/22, kati ya Julai 2021 hadi Mei 2022, jumla ya mikataba 20 inayohusisha miradi ya ujenzi wa Barabara na Viwanja vya Ndege inayogharimiwa moja kwa moja na fedha za ndani na mingine kugharimiwa kwa fedha za Washirika wa Maendeleo ilisainiwa. " amesema

Mwisho. 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.