RC SENYAMULE AHIMIZA WANANCHI WA DODOMA KUHUDHURIA KWENYE TUKIO LA UZINDUZI WA MATOKEO YA SENSA.



Na Rhoda Simba, Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wakazi wa Dodoma kuhudhuria kwa wingi Oktoba 31,2022  katika Viwanja vya Jamhuri Kushuhudia  Uzinduzi wa Matokeo ya Mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi iliyofanyia Agosti 23 2022.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini  Dodoma Senyamule amesema ni vyema kushiriki kwenye uzinduzi huo kwani zoezi hilo ni la kihistoria na hufanyika kila baada ya miaka 10.

"Ni siku ya kipekee na hapa tuna siku moja kufika siku ya kutangaziwa matokeo na Mhe. Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Nitoe shime wana Dodoma mje Kwa wingi kuanzia saa 12 asubuhi hapa kwenye viwanja vya Jamhuri,'' amesema 

"Leo saa 6 usiku tutakuwa na shamla shamla ya kupiga Fataki zikiashiria kuwa Dodoma tupo tayari kuletewa matokeo ya sensa ya watu na makazi hivyo tujitokeze Kwa wingi wana Dodoma" ameongeza Senyamule 

Uzinduzi wa Matokeo hayo yamebebwa na kauli mbiu isemayo "Matokeo ya Sensa ya Sita 2022 Mipango Jumuishi kwa Maendeleo Endelevu"

Mwisho

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.