Rais Samia,Rais Mwinyi na Marais wastaafu kutunukiwa tuzo maalum kwa kufanikisha Sensa...

 


Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu  Sera ,Bunge na Uratibu George Simbachawene amesema Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanzibar Dkt. Hussein Ali Mwinyi pamoja na Marais wastaafu watatunukiwa tuzo maalum kwa kufanikisha Sensa katika vipindi vya uongozi.  

Amezungumza hayo leo Jijini, Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kuelekea kwenye Uzinduzi wa Matokeo ya Mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 utakao fanyika katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Oktoba  31 Oktoba, 2022 .

"Katika uzinduzi huu  Mgeni Rasmi atakuwa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. Sensa ya Watu na Makazi hufanyika mara moja kila baada ya miaka kumi na matokeo yake ndio yanayotumika katika kufanya maamuzi yote muhimu yanayohusu maendeleo ya nchi kwa kipindi cha miaka kumi hadi Sensa nyingine." amesema Simbachawene

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma kuelekea kwenye uzinduzi wa Matokeo ya Mwanzo ya Sensa ya Watu na Makazi 2022.


Aidha, amesema Rais Samia pia  atazindua Mwongozo Maalum wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 lengo lake kuu ni kuhakikisha matokeo ya Sensa yanatumika kwa malengo yaliyokusudiwa. 

"Matokeo haya ni muhimu sana kwa makundi yote katika jamii, wafanyabiashara, wakulima, wafugaji na hasa kwa Serikali yetu inayoongozwa na Rais  Samia  kwani Serikali itaweza kupanga mipango yake kwa ajili ya maendeleo ya wananchi kulingana na idadi, mahitaji na mazingira wanamoishi." ameongeza Simbachawene 

Viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo mawaziri na manaibu waziri, Makatibu wakuu na Manaibu Makatibu Wakuu wa Serikali zetu zote mbili, Wabunge , Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi, Zanzibar, viongozi wa vyama vya Siasa na wawakilishi wa makundi mbalimbali katika jamii watashiriki katika tukio hilo.

 

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.