MAKAMU WAPILI WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR ASEMA MAANDALI YA UZINDUZI MATOKEO YA SENSA YAFIKIA ASILIMIA 85.
Na Rhoda Simba,Dodoma
MAKAMU wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Hemed Mohamed Abdullah amesema kuwa maandalizi ya uzinduzi wa matokeo ya mwanzo ya sensa ya watu na makazi yaliyofanyika tarehe 23 Agosti 2022 yamefikia asilimia 85 ambapo mgeni rasmi wa hafla hiyo anatarajiwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza Jijini Dodoma katika maandalizi ya hafla hiyo yatakayofanyika Oktoba 31 katika uwanja wa Jamhuri amesema kuwa sensa ya mwaka huu ni yakipekee na ya kisasa Kwa sababu imefanyikia kidigitali.
"Sensa ya mwaka huu ni ya kisasa na yakipekee sababu imefanyikia kidigitali kuliko sensa za awamu yote na takwimu hizi zitatusaidia katika maendeleo mbalimbali ya kiuchumi,"amesema.
Kadhalika amesema kuwa sensa hiyo haitatumika Tanzania pekee bali itatumika kwa nchi nyingi duniania kwakuwa tumekuwa tukishirikiana na Nchi mbalimbali katika mambo tofauti tofauti.
Sambamba na hayo amesema takwimu za matokeo ya sensa zitasaidia Kwa kiasi kikubwa shughuli za kiuchumi na kijamii ili kupanga maendeleo kwa maslahi ya Taifa.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema maandalizi ya yanaendelea vizuri ambapo wameunda kamati 11 zinazoongozwa na Wakuu wa Wilaya .
Amesema kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na vyombo vingine wamehakikisha suala hilo linapewa kipaumbele siku hiyo ya tukio.
"Kiujumla tuko vizuri tumeunda kamati 11 na zinaongozwa na wakuu wa Wilaya, kubwa zaidi ni kuhakikisha wanawahamasisha wananchi katika maeneo yao siku hiyo wafike uwanjani mapema kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo,"amesema.
Mwisho.
Huku Mkuu wa Wilaya ya Kongwa
ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Itifaki na mapokezi Remedius Mwema
amesema kuwa mpaka sasa tayari mabalozi kutoka Nchi mbalimbali 20
wamethibitisha kushiriki katika zoezi hilo na pia bado wanaendelea kutoa
mialiko ya viongozi watakao hudhuria na wageni kutoka Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar wakiwemo viongozi na wananchi zaidi ya 140.
Amesema kuwa viongozi na
wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania watahudhuria uzinduzi huo sababu
sensa hiyo ni yakipekee.
Mwisho
Comments
Post a Comment