MAKAMU WAPILI WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR ASEMA MAANDALI YA UZINDUZI MATOKEO YA SENSA YAFIKIA ASILIMIA 85.

 

Na Rhoda Simba,Dodoma 

MAKAMU wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  Hemed Mohamed Abdullah amesema kuwa  maandalizi ya uzinduzi wa matokeo ya mwanzo ya sensa ya watu na makazi yaliyofanyika tarehe 23 Agosti 2022  yamefikia asilimia 85 ambapo mgeni rasmi wa hafla hiyo anatarajiwa kuwa Rais Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza Jijini Dodoma katika maandalizi ya hafla hiyo yatakayofanyika Oktoba 31 katika uwanja wa Jamhuri amesema kuwa sensa ya mwaka huu ni yakipekee na ya kisasa Kwa  sababu imefanyikia kidigitali.

"Sensa ya mwaka huu ni ya kisasa na yakipekee sababu imefanyikia kidigitali kuliko sensa za awamu yote na takwimu hizi zitatusaidia katika maendeleo mbalimbali ya kiuchumi,"amesema.

Kadhalika amesema kuwa sensa hiyo haitatumika Tanzania pekee bali itatumika kwa nchi nyingi duniania kwakuwa tumekuwa tukishirikiana na Nchi mbalimbali katika mambo tofauti tofauti.

Sambamba na hayo amesema takwimu za matokeo ya sensa zitasaidia Kwa kiasi kikubwa shughuli za kiuchumi na kijamii ili kupanga maendeleo kwa maslahi ya Taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema maandalizi ya  yanaendelea vizuri ambapo wameunda kamati 11 zinazoongozwa na Wakuu wa Wilaya .

Amesema kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na vyombo vingine wamehakikisha suala hilo linapewa kipaumbele siku hiyo ya tukio.

"Kiujumla tuko vizuri tumeunda kamati 11 na zinaongozwa na wakuu wa Wilaya, kubwa zaidi ni kuhakikisha wanawahamasisha wananchi katika maeneo yao siku hiyo wafike uwanjani mapema kwa ajili ya kukamilisha zoezi hilo,"amesema.

Mwisho.

 

Huku Mkuu wa Wilaya ya Kongwa ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Itifaki na mapokezi  Remedius Mwema amesema kuwa mpaka sasa tayari mabalozi kutoka Nchi mbalimbali 20 wamethibitisha kushiriki katika zoezi hilo na pia bado wanaendelea kutoa mialiko ya viongozi watakao hudhuria na wageni kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwemo viongozi na wananchi zaidi ya 140.

 

Amesema kuwa viongozi na wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania watahudhuria uzinduzi huo sababu sensa hiyo ni yakipekee.

 

Mwisho 

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.