MAKAMU WA KWANZA WA RAIS ZANZIBAR AITAKA WIZARA YA MAMBO YA NJE KUONGEZA UELEWA KWA WATANZANIA KUHUSU MAMBO YANAYOENDELEA KATIKA JUMUIYA YA KIMATAIFA

 

 


MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, ameitaka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikikiano wa Afrika Mashariki kuongeza uelewa kwa wataanzania kuwezesha kuyafahamu masuala mbali mbali muhimu yanayoendelea katika jumuiya za Kimataifa na Kikanda.

Mhe. Othman ameyasema hayo ofisini kwake Migombani mjini Zanzibar alipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stergomena Tax alieyefika Ofisini kwa Makamu kujitambulisha baada ya uteuzi uliofanywa hivi karibuni na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Makamu amesema kwamba yapo masuala mengi na muhimu yanayoendelea katika Jumuiya hizo ambayo watanzania wa kawaida pamoja na viongozi wanapaswa kuyafahamu katika hatua za michakato hadi utekelezaji wake kwa mafunufaa ya watanzania wote.

Mhe. Othman amefahamisha kwamba kufanya hivyo pia ni muhimu kwani kutasaidia wananchi na Viongozi nchini kuzifahamu fursa mbali mbali za kiuchumi na kimaendeleo zilizopo katika ngazi ya kikanda na kimataifa ili waweze kuzitumia kwa faida yao na taifa kwa jumla.

Mhe. Othman ametolea mfano wa Jumuiya ya Kimataifa inayoshughulikia Haki Miliki za Wabunifu Duniani (WIPO), kwamba zipo fursa nyingi ambazo kutokana na kukosekana uwelewa kwa wananchi fursa hizo hazitumiki ipasavyo na pia kukosekana uwakilishi wa kuchangia masuala mbali mbali pale inapohitajika.

Akizungumzia suala la Balozi mbali mbali zilizoko katika Kituo cha Kenya ambazo uwakilishi wao pia unafikia Tanzania, kuhakikisha kwamba shughuli na huduma zao wanazotoa zikiwemo za watalii wainafikia Zanzibar ili nchi kuweza kunufaikia kupitia kuwepo kwao Tanzania.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stergomena Tax, amesema kwamba wizara hiyo itayafanyia kazi maelekezo aliyopewa na kwamba suala laushirikishwaji wa wananchi katika kujenga uwelewa litawekewa mpango maalumu katika utekelezaji wake.

Amefahamisha kwamba hatua hiyo ni muhimu katika kurahisisha utekelezaji wa masuala mbali mbali yanayotokana na Jumuia za Kikatanda na Kimataifa ambayo nchi imeridhia itifaki zake na pia kusainiwa na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutekelezwa nchini.

Akizungumzia suala la mikutano ya mabalozi inayofanyika Tanzania , Waziri Tax amesema kwamba wizara hiyo itahaikisha kuwepo kwa uwiano sawa kwa pande mbili za muungano katika masuala mbali mbali yanayotekelezwa kupitia itifaki za kibalozi.

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.