HOSPITAL YA BENJAMINI MKAPA YAOKOA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 4.43 KWA WAGONJWA AMBAO WANGETIBIWA NJE YA NCHI
Na Rhoda Simba Dodoma
IMEELEZWA kuwa Hospital ya Benjamin Mkapa (BMH) imefanikiwa kupandikiza
figo kwa watu 31 nakuokoa fedha kiasi cha zaidi ya shilingi bil 2.3 huku
ikitibu watu 715 ugonjwa wa moyo na kati yao 39 walibainika na matatizo ya moyo
nakuwekewa vipandikizi na kati yao 8 wamepandikiziwa betri kwenye moyo.
![]() |
Dkt. Alphonce Chandika |
Hayo yameelezwa Leo na Dkt. Alphonce Chandika Mkurugenzi Mtendaji wa (BMH) wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu ya hospitali hiyo na mwelekeo wa mwaka wa fedha 2022/ 2023 amesema watoto 14 waliozaliwa na shida ya moyo wametibiwa huku watoto 10 wakifunguliwa vifua na kufanyiwa upasuaji.
“Uwepo wa maabara hii ni uwekezaji muhimu wa kuokoa maisha ya wananchi
hususani hapa makao makuu ya nchi kwahiyo tuna wananchi wawili ambao walihudumiwa
kwa dharula na wakaokolewa maisha yao kuna baadhi ya wagonjwa ambao mapigo yao
huwa yanaenda taratibu na chini hivyo huwa tunawawekea betri ya kuongeza mapigo
ya moyo na kupitia maabara hii huwa tumeweza kuhudumia watoto waliozaliwa na
matatizo ya matundu ya moyo” amesema Dkt Chandika
Aidha Dkt Alphonce amesema Bilioni 1.28 zimeokolewa kwa kuwafanyia
upasuaji wagonjwa 58 wa nyonga kwakuwawekea vipandikizi kwa gharama ya shilingi
milioni 12 badala yakutibiwa nje ya nchi kwakiasi cha shilingi milioni 35 kwa
mgonjwa mmoja.
“ukiangakia kwa hawa wagonjwa 56 tumeweza kuokoa jumla ya shilingi
Bilioni 1.28 za kitanzania ambapo pesa hizo zilitakiwa zikawatibie hawa watu
nje ya nchi Amesema Dkt Chandikwa
Katika hatua nyingine mkurugenzi huyo amesema bmh imeanza kutoa mafunzo
kwa wataalamu wa usingizi na ganzi na tayari wataalamu 127 wamehitimu huku
akibainisha kuwa hospiltal hiyo inakwenda kuongeza wigo wa huduma kwakujenga
jengo maalum kwaajili ya matibabu ya moyo, upasuaji wa mifupa na ubongo ili kuhakikisha
hospital hiyo inakuwa ya pili ya taifa.
“Tunatarajia hizi huduma pia tuweze kujenga jingo kubwa kwaajili ya ya
huduma za ugonjwa wa moyo maana ndio yanakuja kwa kasi tunatarajia mpaka elfu
mbili ishirini na tano tuwe tumekamilika" amesema Dkt. Chandikwa
Mwisho
Comments
Post a Comment