ZAIDI YA WATU 60,000 DUNIANI HUFARIKI KWA KICHAA CHA MBWA KILA MWAKA

 



Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Takwimu zinaonesha kwamba watu zaidi ya 60,000 hufariki kwa kichaa cha mbwa duniani kila mwaka huku Kwa Tanzania, wastani wa matukio ya majeraha kwa binadamu yanayotokana na kuumwa na mbwa ni 3,387 kila mwaka.

Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya siku ya kichaa cha mbwa duniani yaliyofanyika kitaifa kata ya Mpunguzi leo jijijini Dodoma, Mkuu wa mkoa Rosemary Senyamule amesema Kwa mujibu wa ripoti ya WHO mwaka 2017, ugonjwa wa kichaa cha mbwa husababisha wastani wa vifo vya binadamu 1,500 kila mwaka nchini Tanzania.

Mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule 


‘’Takwimu zaidi zinaonesha kuwa watoto chini ya umri wa miaka 15 ndiyo hupatwa zaidi na madhara haya kwa kuwa na ukaribu na urafiki na mbwa.’’ amesema Senyamule

Aidha, amesema kwa hapa Tanzania, kila mwaka kuna wastani wa matukio 2,030 ya mbwa wanaodhaniwa kuwa na kichaa.

‘’Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Afya za Wanyama Duniani (WOAH) and Shirika la Chakula na Kilimo (FAO) kwa pamoja yamekubaliana kutokomeza ugonjwa wa kichaa cha mbwa ifikapo 2030. Njia ya kuu ya kufikia malengo haya ya dunia ni chanjo kwa mbwa wote kila mwaka (annual massive vaccination), kupunguza idadi ya mbwa, kuzingatia ufugaji bora wa mbwa ikiwa ni pamoja na kufungia mbwa wasizurure mitaani.’’ameongeza Senyamule

Mbali na hilo, amesema Kwa Tanzania, ina Mkakati wa Kitaifa wa Kutokomeza Ugonjwa wa Kichaa cha Mbwa wa mwaka 2019 (National Rabies Control strategy, 2019).



‘’Lengo lake ni kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha mbwa na hatimaye kuutokomeza kabisa ifikapo 2030. Pia, kuna Mpango Mkakati wa Afya Moja (2015-2020) unaotoa wajibu wa kila mmoja katika kudhibiti ugonjwa wa kichaa cha mbwa kwa njia ya chanjo.’’ amesisitiza Senyamule 

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga amesema watahakikisha mbwa wote wanachanjwa ili kuwakinga na ugonjwa huo.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Hezron Nonga 


‘’Natoa wiito kwa wananchi tuhakikishe kwamba tunachanja mbwa wetu katika hii wiki lakini kwa muda wa mwaka mzima .  Kwa sababu kalenda ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa ni kuanzia mwezi wa kwanza mpaka mwezi wa 12.’’

Perez Rumolwa aliyebahatika kuhudhuria katika maadhimisho ya kilele hicho, amesema ugonjwa wa kichaa cha mbwa huweza kusababisha kifo ikiwa mtu hatowahishwa hospitali huku akiishukuru Serikali kwa kutoa chanjo hizo . 

Ndugu yangu mwenyewe, alikuwa binamu aling’atwa na mbwa ikasababisha kifo chake.’’

Hapa nchini, kuna takribani mbwa milioni 4.5 na paka milioni 2 wanaofugwa kwa malengo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ulinzi, kusaidia kuchunga mifugo na uwindaji.

Mwisho. 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.