WANANCHI JIJI LA DODOMA WAELEZWA FAIDA ZA USHURU WA HUDUMA

Na. Getruda Shomi, DODOMA

MHASIBU wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Theresia Cosmass aeleza faida za ushuru wa huduma kwa wananchi na wafanyabiashara kuwa ni kusaidia Halmashauri kupata mapato yatakayotekeleza miradi ya kimaendeleo na kuimarisha huduma za kijamii.

Theresia Cosmass


Alisema hayo alipokuwa katika oparesheni ya kukusanya mapato katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, kata ya Ihumwa Mtaa wa Flamingo, ikiwa ni siku ya pili ya oparesheni hiyo.

Cosmass alisema kuwa ushuru wa huduma ni muhimu kwani hupelekea maboresho ya miundombinu na kuimarisha huduma za kijamii ambapo itasaidia wananchi kupata huduma nzuri na kwa urahisi.

“kodi ya ushuru wa huduma itasaidia kuboresha huduma za kijamii kama hospitali, ujenzi wa barabara na kwa wafanyabiashara miundombinu ya barabara ambayo itasaidia biashara zao kufikika kwa urahisi” alisema Cosmass.

Naye Afisa Biashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Amri Kibwana aliongeza kuwa mwitikio wa operesheni hiyo ni chanya na wafanyabiashra wanachukua hatua kama inavyoelekeza sheria baada ya kupatiwa elimu.

“Pale tunapokuta mapungufu, tunatoa elimu na kuwapa maelekezo namna ya kuanza mchakato wa kulipa ushuru wa huduma na wafanyabiashara wanamwitikio mzuri wanakuja ofisini kwaajili ya kufanya malipo” alisema Kibwana.

Akitoa wito kwa wafanyabiashara wengine, Sospeter Kanichi amabae ni mfanyabiashara wa bucha ya nyama alisema kuwa wafanyabiashara wafuate maelekezo kwa kulipa ushuru wa huduma kwasababu ni njia majawapo ya kuchangia maendeleo ya nchi.

Sospeter Kanichi


“Ni sahihi kulipa ushuru wa huduma kwasababu tunachangia serikali yetu na tunaboresha nchi yetu lakini pia biashara zetu. Hivyo, watu wasikimbie” alisema Kanichi.

Oparesheni hiyo iliyoanza jana itadumu kwa siku tatu na baadae itafanyika oparesheni kwaajili ya kukagua utekelezaji.

 

MWISHO

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.