NIC : TUMETENGENEZA FAIDA YA ZAIDI YA BILIONI 73 KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2020/2021...

 


Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Shirika la Bima la Taifa (NIC ) limesema kuwa limeweza kutengeneza faida ya zaidi ya bilioni 73  katika kipindi cha mwaka 2020/2021 kutokana na watu kukata bima za mali, ajali na maisha .

Hayo, yalielezwa Septemba 29, 2022 katika Mkutano wa Chama cha Mawakili wa Serikali na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la hilo Karim Meshack alisema, Shirika  mwanzo lilikuwa haliwezi kutengeneza faida, lilikuwa likiendeshwa kwa hasara.


 ‘’Lakini kwa miaka minne mfululizo limekuwa likiendeshwa kwa faida. Na kwa mfano rekodi ya mwaka 2020/2021 tumeweza kutengeneza faida ya zaidi ya bilioni 73 . ‘’alisema 

Aidha, alisema utengenezaji wa faida wa shirika hilo imetokana na Shirika kufanya mapinduzi katika maeneo makubwa matatu ikiwemo eneo la rasimali watu.

‘’Kwa maana tumetafuta wataalam wenye weledi wa kuweza kuliendesha Shirika. Kwenye eneo hilo hilo la rasimali watu, ni pamoja na kupata vijana wenye weledi wa kuweza kufanya biashara.’’ aliongeza

Akitaja eneo lingine , alisema ni eneo la kimfumo ambapo Shirika limekuwa likiendeshwa kidigitali kwa maana ya mifumo ya tekinolojia ya habari. ‘’ Sasa hivi ukija kwenye Shirika hauwezi kukutana na karatasi. Shughuli zote za bima zinafanyika kwenye mfumo .’’ alisema 

‘’Lakini, eneo la tatu ni la kiubunifu . Tumetengeneza upya bidhaa zetu zote za kibima .Kwa hiyo tumekuwa na bidhaa nyingi ambazo zinajibu changamoto za wateja wetu. Watu wanatakiwa kuja kutupa ushirikiano,kupata huduma za bima  .’’ alisisitiza

Shirika hilo, limewashauri watanzania mbalimbali kujitokeza kulitumia  kwani lina manufaa makubwa  na litawasiadia kujikinga na majanga mbalimbali endapo yatatokea.

Mwisho. 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.