CHANDE: WADAU NA WATUMISHI MNAOHUSIKA NA UNUNUZI WA UMMA MZINGATIE SHERIA MSILIINGIZE TAIFA KWENYE HASARA

 


Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Hamad Hassan Chande, ametoa wito kwa wadau wote na watumishi wanaohusika na ununuzi wa Umma kuzingatia sheria na miongozo ili kutoingiza Taifa katika hasara.

Chande ameyasema hayo leo jijini Dodoma, wakati akipokea Ripoti ya Tathmini ya Utendaji katika Ununuzi wa Umma PPRA  mwaka 2021/2022.

‘’Tutaendelea kuchukua hatua kali kwa kadiri tunavyowabaini. katika utendaji kazi katika ununuzi wa umma, kuzingatia mambo makuu manne ambayo kwenu yatakuwa ni msingi wa utendaji bora katika ununuzi. Moja ni uwajibikaji ,mbili ni uwazi, tatu utawala bora na thamani ya fedha.’’

Aidha, Naibu Waziri huyo ameipongeza PPRA kwa kuhakikisha kuwa inafanya kazi zake kwa umakini na kufuata sheria na miongozo mbalimbali inayotolewa na Serikali.

Naibu Waziri Wizara ya Fedha na Mipango  (kulia) Hamad Hassan Chande akipokea Ripoti ya Tathimini ya Utendaji katika Ununuzi wa Umma PPRA 2021/2022 kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurungezi  PPRA Dkt. Leonada Mwagike (kushoto)


‘’Itakumbukwa, katika wasilisho langu la bajeti bungeni kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 nilitoa maelekezo kwa Wizara yangu kuhakikisha inasimamia mchakato wa uboreshaji wa Sheria ya Ununuzi wa Umma, Sura Na. 410, kazi ambayo nimetaarifiwa kuwa tayari imeshaanza na hivi karibuni wataweza kuwasilisha mapendekezo kwa ajili ya hatua nyingine.’’

Katika hatua nyingine, amesema PPRA imekuwa na mchangao mkubwa katika kusimamia ununuzi kwenye miradi ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) na Mradi wa Kufua Umeme wa Mwalimu Nyerere (MNHPP).

‘’Nasikitika kuona bado baadhi ya taasisi hazikidhi matakwa ya Sheria ya Ununuzi wa Umma hivyo kurudisha nyuma juhudi za kuleta maendeleo zinazofanywa na Serikali. Nitakaa pamoja na viongozi wa wizara yangu na wa PPRA ili kuona namna bora ya kushughulika na hizo taasisi zote zilizoshindwa kukidhi matakwa ya sheria.’’

Sambamba na hayo amesema, kumekuwepo na ubadhirifu mkubwa wa fedha za Umma wakati wa ununuzi kwa kutokuwa na weledi na uaminifu.

‘’Mathalani ukilinganisha bei ya bidhaa na huduma sokoni na bei inayonunua Serikali zinatofautina kwa kiasi kikubwa sana. Fedha nyingi za Serikali zinapoteza kwa mtindo huu.’’

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurungezi ya PPRA Dkt. Leonada Mwagike Licha ya uwepo wa mfumo huu wa ununuzi, zimeonekana changamoto kadhaa kiasi cha kuifanya Serikali iamue kujenga mfumo mpya wa ununuzi.

‘’Changamoto hizo ni pamoja na Mfumo wa TANePS hauna uwezo wa kulazimisha Taasisi nunuzi zinapofanya manunuzi kuchakata mpaka mwisho zabuni zao ndani ya mfumo, Mfumo kutokuwa na uwezo wa kujumuisha bei elekezi ili kudhibiti gharama za ununuzi na kusaidia Serikali kupunguza gharama za ununuzi,’’

‘’Mfumo kutokuwa rafiki kwa watumiaji. Hii ni kutokana na mfumo kuhitaji watumiaji wapandishe (upload) taarifa nyingi katika nakala ngumu. Baadhi ya moduli kutokamilika hadi kufikia Mwezi Julai 2022, Gharama za kuendesha mfumo na kufanya maboresho pale inapohitajika ni kubwa na Kandarasi ya mfumo kufikia ukomo ifikapo mwezi Disemba

2023.’’

Ripoti hiyo , iliyowasilishwa inatoa tathmini ya utendaji kwa kuelezea majukumu mbalimbali yaliyotekelezwa na Mamlaka katika Mwaka wa Fedha 2021/2222.

Majukumu hayo ni pamoja na  Kutoa huduma za ushauri katika ununuzi wa umma, Maelezo ya Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Kujenga uwezo kwa taasisi katika kutekeleza Sheria ya Ununuzi wa Umma,Kutekeleza mfumo wa ununuzi kwa njia ya kielektroniki na Kusimamia Sheria ya Ununuzi wa Umma.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.