Na Mwandishi Wetu
Kilimanjaro
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George
Simbachawene ameomba wananchi kuenzi mambo mema yaliyoachwa kama alama
wakati wa uhai wa Mhe. Augustino Lyatonga Mrema.
“Tunamkumbuka
kwa uzalendo wake wa kupenda demokrasia, lakini pia kupenda amani na utulivu
katika itikadi zote. Mrema ni mtu mwenye rekodi kubwa katika siasa za ushindani
wa nchi yetu”
Hayo
yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe.
George Simbachawene akitoa salamu za serikali katika ibada ya mazishi ya
hayati Augustino
Lyatonga Mrema iliyofanyika Marangu – Vunjo Mkoani Kilimanjaro.
"Sisi
kama serikali tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu; kushiriki msiba kwa
moyo mkuu maana sisi sote tunakwenda safari hiyo, yeye ametangulia sisi
tupo nyuma yake, alisema waziri."
Ameeleza
serikali na viongozi wakuu wanawapa pole Mama Watoto wa Marehemu na
Wanakiraracha kwa ujumla na kipekee sana wanachama wote wa TLP, chama
ambacho amefariki akiwa ni Mwenyekiti wake wa Kitaifa.
“
Marehemu Mrema amefariki akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole,na
amefanya kazi yake vizuri alisema Waziri”
Akitoa
salamu za pole kwa niaba ya Mhasham Baba Askofu Ludovick Minde, Askofu wa Jimbo
Katoliki la Moshi, Padre Deogratius Matiika wakili wa Askofu Jimbo Katoliki
Moshi ametoa pole kwa wanafamilia na wale wote walioguswa na msiba.
Sisi
kazi yetu kubwa ni kuendelea kumuombea ili Mwenyezi Mungu ampe furaha mbinguni,
ameshiriki na sisi katika maendeleo ya jimbo letu, na tunashukuru Mungu kwa
hayo aliyoyafanya.
“Nawaomba
wanafamilia Mshikamane baba ameondoka msije mkagombana, mkae kwa amani na
upendo, alisema Padre Matiika”
Comments
Post a Comment