Waziri Simbachawene; tuenzi mambo mema yalioachwa na Mrema

 


Na Mwandishi Wetu Kilimanjaro

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene ameomba wananchi kuenzi mambo mema yaliyoachwa kama alama wakati wa uhai wa Mhe.  Augustino Lyatonga Mrema.

“Tunamkumbuka kwa uzalendo wake wa kupenda demokrasia, lakini pia kupenda amani na utulivu katika itikadi zote. Mrema ni mtu mwenye rekodi kubwa katika siasa za ushindani wa nchi yetu”

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene akitoa salamu za serikali katika ibada ya mazishi ya hayati Augustino Lyatonga Mrema iliyofanyika Marangu – Vunjo Mkoani Kilimanjaro.

"Sisi kama serikali tunaungana nanyi katika wakati huu mgumu; kushiriki msiba kwa moyo mkuu maana sisi sote  tunakwenda safari hiyo, yeye ametangulia sisi tupo nyuma yake, alisema waziri."

Ameeleza serikali na viongozi wakuu wanawapa pole Mama Watoto wa Marehemu na Wanakiraracha kwa ujumla na kipekee sana wanachama wote  wa TLP, chama ambacho amefariki akiwa ni Mwenyekiti wake wa  Kitaifa.

“ Marehemu Mrema amefariki akiwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole,na amefanya kazi yake vizuri alisema Waziri”

Akitoa salamu za pole kwa niaba ya Mhasham Baba Askofu Ludovick Minde, Askofu wa Jimbo Katoliki la Moshi, Padre Deogratius Matiika wakili wa Askofu Jimbo Katoliki Moshi ametoa pole kwa wanafamilia na wale wote walioguswa na msiba.

Sisi kazi yetu kubwa ni kuendelea kumuombea ili Mwenyezi Mungu ampe furaha mbinguni, ameshiriki na sisi katika maendeleo ya jimbo letu, na tunashukuru Mungu kwa hayo aliyoyafanya.

“Nawaomba wanafamilia Mshikamane baba ameondoka msije mkagombana, mkae kwa amani na upendo, alisema Padre Matiika”

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.