Na Mwandishi wetu- Dodoma
Wakristo
nchini wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kujietea maendeleo, changia pato
la Taifa na kutatua changamoto zilizo katika maeneo yao.
Hayo
yameelezwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe.
George Simbachawene wakati akizunguma katika sherehe ya kumweka wakfu Askofu
wa tatu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya Mpwapwa, Rev. George
Chiteto iliyofanyika Jijini Dodoma baada ya aliyekuwa askofu wa kanisa hilo
Askofu Donald Mtetemela kumaliza muda wake .
Waziri
Simbachawene alisema chanamoto nyngi za kiuchumi katika jamii zitatauliwa
endapo wananchi watajituma kufanya kazi na kuwa wabunifu kwa
kuanzisha miradi mbalimbali kama ambavyo maandiko matakatifu yanaagiza watu
kufanya kazi.
“Lazima
wakristo wa sasa tufanye kazi lazima tutae changamoto kwenye maeneo yetu maana
imeandikwa katika biblia asiyefanya kazi na asile kwahiyo kufanya kazi ndio
uhai wako, heshima yako na ukizalisha utaweza kuendesha maisha yako binfasi,
utashiriki katika kazi ya Mungu na Taifa zima,” alisema Waziri Simbachawene.
Pia
aliongeza kwamba serikalii itaendelea kushirikiana na taasisi za dini kwani
zimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo, kusimamia maadili na kupambana na
vitendo vya mmomonyoko wa maadili kwa baadhi ya watu wasiyo na hofu ya Mungu.
“Licha
ya mchango mkubwa wa kanisa hili kwa serikali lakini kumekuwa na mmomonyoko wa
maadili, magonjwa na majanga mbalimbali hivyo ni muhimu kushirikiana na
serikali ili kuokoa vijana na watoto wetu na ni matumaini yetu viongozi wa dini
mkiendelea kusimama imara na kutoa huduma ya kiroho tutatatua
changamoto hii,” alieleza.
Aidha
alibainisha kwamba Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais
Samia Suluhu Hassan imeendelea kuchukua hatua za kisheria kwa watu wote
wanaojihusisha na vitendo vya rushwa , ufisadi, utovu wa nidhamu kwa watumishi
wa umma pamoja na jamii kwa ujumla.
Kwa
upande wake Askofu Mkuu wa Kanisa Anglikana Tanzania Mhashamu Dr. Maimbo
Mndolwa aliipongeza serikali kwa kuwa mstari wa mbele kuziunga mkono
taasisi za dini katika nyanja zote huku akimtaka Askofu Chiteto kufanya
kazi kwa kumtegemea Mungu hatimaye kufikia malengo ya kanisa.
Naye
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule alitoa wito kwa wakazi
wa mkoa huo kutumia fursa ya serikali kushusha bei ya mbolea kwa
kujikita katika kilimo.
Comments
Post a Comment