Mkoa wa Ruvuma wafikia asilimia 63 ya lengo la kuhesabu kaya 450,000

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Laban Thomas amesema takwimu ya kitaifa ya sensa inaonesha kuwa hadi kufikia Agosti 26 mwaka huu saa moja asubuhi Mkoa wa Ruvuma ulikuwa umefikia asilimia 63 ya lengo la Kuhesabu zaidi ya kaya 450,000.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas alipowasili katika ofisi za Mtendaji Kata ya Peramiho Halmashauri ya Songea kwa ajili ya ukaguzi wa zoezi la sensa katika baadhi ya mitaa ya  Kata hiyo


Kanali Thomas amesema hayo wakati anazungumza na wananchi wa Peramiho nje kidogo ya Mji wa Songea alipofanya ziara ya kukagua zoezi la sensa linaloendelea nchini kote.

Amesema kutokana na takwimu hizo za kitaifa Mkoa unakwenda vizuri ambapo ametoa rai kwa wananchi kuendelea kushirikiana na makarani kwa kujitokeza kuhesabiwa ili Mkoa uweze kupata takwimu za sensa za watu za kutosha ambazo zitaisaidia serikali kupanga mipango ya maendeleo.

Hata hivyo Kanali Thomas amesema anatamani Mkoa wa Ruvuma uvunje rekodi za kitaifa kwenye majumuisho ya sensa kwa kuongoza kitaifa.

RC Thomas amewapongeza watendaji  kwa usimamizi mzuri katika zoezi la sensa  ambapo amewataka viongozi wa Halmashauri zote kuendelea  kuwaelimisha wananchi wajitokeze kuhesabiwa ili kufikia malengo ya Mkoa na taifa kwa ujumla

“Matumaini yangu tuakwenda vizuri  niwaombe wananchi wenzangu endeleeni kujitokeza ili tupate data sahihi, data hizi zina manufaa  kwetu na kwa taifa letu”alisema RC Thomas.

Naye Mkurugenzi wa Halmashaur ya Wilaya ya Songea  Neema Maghembe ameeleza Halmashauri  hiyo yenye Kata 16, inatarajia kuhesabu kaya  zaidi ya 36,000,  na kwamba hadi   kufikia Agosti, 25,  wameweza kuhesabu kaya zaidi ya 28,000.

“Nikuhakikishie Mkuu wa Mkoa zoezi hili linakwenda vizuri na watu wanajitokeza kuhesabiwa, hata kaya uliotembelea umekuta zoezi linakwenda vizuri” alisema Bi maghembe.

Mkoa wa  Mkoa wa Ruvuma, anaendelea na ziara ya  kukagua  maendeleo ya zoezi la sensa ya watu na makazi katika Halmashauri za Mkoa wa Ruvuma.Zoezi hili  lilianza  Agosti, 23, 2022 na linatarajiwa kukamilika Agosti, 28 mwaka huu.

Imeandikwa na Albano Midelo

Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Mkoa wa Ruvuma

Agosti 26,2022


Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Thomas Laban akizungumza na wananchi  wa Mtaa wa Peramiho ambao tayari walikuwa wamehesabiwa katika zoezi la sensa ambalo linaendelea nchini kote




Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas akiwa na wajumbe wa Kamati ya Sensa Mkoa na Halmashauri ya Wilaya ya Songea  akitembea katika baadhi ya mitaa kukagua mwenendo wa zoezi la sensa ambalo lilianza Agosti 23 na linatarajia kukamilika Agosti 28




Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Thomas Laban akizungumza na wananchi  wa Mtaa wa Peramiho ambao tayari walikuwa wamehesabiwa katika zoezi la sensa ambalo linaendelea nchini kote


 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.