JAFO AAGIZA OPARESHENI KABAMBE TOKOMEZA MIFUKO YA PLASTIKI

Na. Rhoda Simba, DODOMA

 

KATIKA kutekeleza agizo la Makamu wa Rais, Dkt. Philp Mpango, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Selemani Jafo ameagiza kuanzishwa kwa oparesheni kabambe yakuteketeza mifuko ya plastiki katika maeneo mbalimbali nchini.

 

Waziri Selemani Jafo

Kadhalika amewaagiza wale wote ambao wamekuwa wakitumia vifungashio kama vibebeo kuacha kufanya hivyo mara moja huku akizitaka kamati za ulinzi za Mikoa na Wilaya kuchukua hatua kwa watakao kiuka.

 

Waziri Jafo ametoa agizo hilo leo Agosti 26 jijini hapa wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa sheria ya mazingira amesema kampeni hiyo itatekelezwa katika maeneo ya maduka, sokoni, magulio, mabucha ya nyama pamoja na samaki.

 

"Tukumbuke kwamba hivi karibuni tumeweza kukamata mizigo mbalimbali katika maeneo na kanda zetu mbalimbali ambapo mizigo mingine imekuwa ikitokea nje ya nchi kwa kukamatwa ikipita Katika mipaka yetu ya nchi,

 

"Jambo hili hali ridhishi hata kidogo kufuatia hilo Makamu wa Rais wa Muungano na Mazingira Dkt.  Philip Isdor Mpango ameeleza kwamba kuanzishwe oparesheni kabambe ya kuhakikisha kwamba hakutaonekana tena mifuko ya plastiki katika mitaa yetu hili ni agizo la Makamu wa Rais wa Tanzania Dkt. Philp Isdor Mpango" amesema Dkt. Jafo.

 

Aidha, ameagiza wakuu wa Mikoa kupitia kamati za usalama kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa pamoja na kudhibiti uingizwaji wa vibebeo hivyo mipakani sambamba na kuwashirikisha viongozi wa masoko kama anavyoeleza.

 

"Nikiwa Waziri mwenye dhamana niagize maeneo yote watu wote tutaenda kufanya kazi site kutekeleza agizo la Makamu wa Rais ambapo jambo la kwanza tuwashirikishe viongozi wa masoko na viongozi wa magulio wao ndio shughuli hizo za vifungashio vinatokea kwao" amesema Dkt. Jafo.

 

Agizo hilo linakuja kufuatia matumizi holela ya vifungashio ambapo baadhi ya maeneo wazalishaji na wasambazaji wa vifungashio wamepeleka vifungashio sokoni kutumika kama kibebeo swala ambalo ni kinyume na hivyo kusababisha uchafuzi wa mazingira na kwenda kinyume na utekelezaji wa Sheria ya mazingira nchini.

 

Mwisho

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.