DKT. PINDI CHANA AHIMIZA UTATUZI WA KERO ZA UHIFADHI NA MIGOGORO BAINA YA WANANCHI

 

 





Na Rhoda Simba Dodoma,

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Dkt. Pindi Chana amewaasa Makamanda,Maafisa na Askari wa Uhifadhi (TFS) kushirikiana na wadau mbalimbali katika kutatua kero za uhifadhi na  migogoro baina ya wananchi .

Akizungumza leo jijini Dodoma katika mafunzo ya makamishina, makamanda na askari wa uhifadhi wa misitu ya kila mwanzo wa mwaka wa fedha, ambapo amewataka kusimamia sheria pamoja na kutowaruhusu wavamizi wasipewe nafasi kuingia katika hifadhi za misitu kwa maendeleo ya Taifa na watu wake.

 

"Nawaelekeza kusimamia sheria na shirikianeni na kamati za ulinzi na usalama za Mikoa na Wilaya kuhakikisha wavamizi wote wanaondoka na kuacha hifadhi za misitu zikiwa salama, ndugu zangu jambo hili la uvamizi katika maeneo ya misitu tusiliruhusu na hili ni eneo ambalo tutawapima" Amesema Dkt Pindi Chana.

 

Aidha,Dkt Pindi Chana amesema ili kuwa na misitu bora nikuilinda na kuihifadhi ili kuziwezesha sekta nyingine kukua huku akiwaomba askari hao kutumia silaha kwa utaratibu mzuri ili kulinda heshima ya jeshi la uhifadhi.

 

"Ndugu viongozi na makamanda nyinyi nyote mnao wajibu wa kulinda na kuendeleza rasilimali za misitu na nyuki,hili ni jukumu la msingi ambalo mbinu za kijeshi zinatakiwa kuwezesha kufikia lengo hili yani kuwa na misitu bora katika kuziwezesha sekta zingine kukua" amesema Dkt Pindi chana.

 

Kwa upande wake Prof.Dos Santos Silayo Kamishna wa uhifadhi Wakala wa huduma za Misitu Tanzania(TFS) ameitaja changamoto ya kuongezeka kwa matishio ya kiusalama na ongezeko la wananchi kujichukulia sheria mkononi jambo ambalo linapelekea kujeruhiwa na kuuawa kwa baadhi ya askari na maafisa wakati wakitekeleza majukumu yao.

 

"Ni changamoto kubwa sana na hizi siku za karibuni matukio haya yamekuwa yakiongezeka, lakini kama jeshi la uhifadhi tumejipanga katika kukomesha vitendo hivi,lakini pia kuongezeka kwa vyombo vya usafiri hususani pikipiki katika maeneo ya uhifadhi nalo pia ni changamoto kubwa sana,na changamoto hii tunaendelea kuifanyia kazi kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali zinazosimamia vyombo hivi" amesema Prof silayo.

 

Hata hivyo dhamira ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) ni kuwa na usimamizi endelevu wa rasilimali za kitaifa za misitu na nyuki ili kuchangia mahitaji ya kijamii, kiuchumi, ki-ikolojia na kiutamaduni kwa kizazi cha sasa na kijacho”.

 

 

 

Mwisho.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.