Na. Sifa Stanley, DODOMA
WAZIRI
wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira, Selemani Jafo ameipongeza
Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa juhudi zake za kuliweka jiji safi.
Waziri Selemani Jafo akishiriki zoezi la usafi wa Mazingira Soko la Bonanza |
Pongezi
hizo alizitoa mapema leo aliposhiriki zoezi la usafi pamoja na wananchi katika Soko
la Bonanza Kata ya Chamwino Halmashauri ya Jiji la Dodoma
“Watu
wa hapa mnafanya usafi kweli, sio kwa kuigiza. Nimetembea maeneo yote katika Samaki,
Ndizi, Viazi pamoja na Matunda nimekuta mmefanya usafi. Ninyi ni watu wa kuigwa
ndani ya Tanzania. Hii inadhihirisha kuwa maagizo ya Rais, Mama Samia na Dkt. Isdory
Mpango akiwa yeye ni Makamu wa Rais na akisimamia upande wa Mazingira na Waziri
Mkuu, wamekuwa wakitoa maelekezo kuhusu Mazingira na kufanya usafi, wanabonanza
nimeshuhudia kwamba ni wasafi sana” alisema Waziri Jafo.
Pia
Waziri Jafo alitoa wito kwa wananchi wa maeneo mengine kuzingatia maelekezo ya Serikali
kuu ya kuacha biashara zao kwa muda mfupi na kufanya usafi siku ya Jumamosi.
Sambamba na hilo alisisitiza watu wa maeneo mengine kuiga mfano wa Dodoma wa
kuendeleza utamaduni wa usafi na kutunza Mazingira ili kuendelea kuiweka Nchi
katika hali ya usafi.
“Niwaombe
maeneo mengine waige mfano wa Dodoma, na Mkurugenzi wetu jambo hili liendelee
katika masoko mbalimbali. Nafahamu wiki iliyopita tulikuwa na ajenda kama hii Soko
la Majengo, leo hii tupo Soko la Bonanza inawezekana huenda Jumamosi ijayo
tutakuwa Soko la Mavunde. Hili linawezekana tuwe tunabadilika, jiji letu
tunafahamu ndio Makao Makuu ya nchi sura ya nchi yetu inapatikana Dodoma. Lazima
tuhakikishe tunafanya usafi. Mimi kama Waziri wa Mazingira Tanzania hapa
nimeridhika mnatunza Mazingira wanabonanza” alisema Jafo.
Nae
Mkuu wa Idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu Halmashauri ya Jiji la
Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa na
utaratibu wa kufanya usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi na kuongeza kuwa Halmashauri
ya Jiji la Dodoma imetenga kiasi cha shilingi milioni 38 kwaajili ya kuboresha Soko
la Bonanza.
“Katika
Jiji la Dodoma tumekuwa tukifanya usafi kwa maelekezo ya mkuu wa mkoa kila Jumamosi
tumekuwa tukifanya usafi isipokuwa Jumamosi ya pili ya mwezi huwa tunaiacha
kwaajili ya maelekezo ya serikali kuu watu kufanya mazoezi. Soko la Bonanza ni
moja kati ya masoko masafi kama alivyosema Afisa Mtendaji Kata ya Chamwino na
Halmashauri ya Jiji la Dodoma imekuwa ikiendelea kuboresha mahali hapa na
tumetenga shilingi milioni 38 kwa mwaka huu wa fedha wa serikali ili kuboresha
soko hili” alieleza Kimaro.
MWISHO
Comments
Post a Comment