SHEKIMWERI APONGEZA JESHI LA POLISI KWA KUHUDUMIA WANANCHI KUPITIA KAMPENI YA AFYA BOMBA.


Na Rhoda Simba, Dodoma.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Jabir Shekimweri amelipongeza Jeshi la Polisi kupitia kituo cha afya Polisi Dodoma kwakujitoa kuhudumia wananchi kupitia kampeni ya afya bomba pima .

 

Kampeni hiyo imeanza leo hadi  Julai 31 ambapo wananchi wanapata huduma ya kupima magonjwa mbalimbali kama vile kisukari, figo, moyo, tezi dume, kinywa na meno pamoja na magonjwa ya kina mama.

 

Akitoa pongezi hizo , Shekimweri amesema mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 30 hiyo ikiwa inaashiria uzalendo kwa manufaa ya umma yenye tija.

 

“Binafsi nmefurahishwa na nimeridhishwa kwamba mmefanya kazi hii kizalendo askari mmetekeleza mradi huu kizalendo. Askari mmetekeleza mradi huu kwa gharama nafuu mimi niwahakishie kwamba tupo tayari kuwaaunga mkono katika ajenda hii kubwa muhimu kwasababu mmeunga mkono jitihada za serikali katika kuwahudumia wananchi masuala ya afya." amesema Shekimweri.

 

Ameongeza kuwa, serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 500 kwaajili yakuanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Nala jijini Dodoma huku akiwasisitiza wananchi kijitokeza kuhesabiwa kwenye zoezi la sensa ya watu na makazi.

 

“ Natoa rai kwa wananchi jitokezeni kwa wingi moja kufanya shughuli za upimaji kwenye kituo cha polisi hapa Dodoma na serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan imetupatia million 500 za kuanza kujenga kituo cha afya Nala na muhimu Zaidi tujitokeze kuhesabiwa ili mipango ya maendeleo ikapangwe vizuri’amesema Shekimweri ." ameongeza Shekimweri 

 

Akisoma risala mtoa huduma wa kituo hicho Redemta Kisima ameelezea changamoto zinazokabili kituo cha afya polisi Dodoma kuwa ni uhaba wa majengo hususani jengo la kujifungulia wakina mama, madaktari bingwa na chumba cha upasuaji.

 

 

“Tunazochangamoto chache zinazotukabili ikiwemo uhaba wa majengo hususani chumba cha kujifungulia, wodi ya wagonjwa mahututi,wodi ya watoto ,wodi ya upasuaji, madaktari bingwa, madaktari wa upasuaji na madaktari wa watoto wauguzi wafamasia na wataalam wa maabara.” amesema Kisima

 

 

Mwisho

 


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.