Kampuni ya TOL Gases inavyoongeza chachu ya maendeleo mkoani Mbeya


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mheshimiwa Juma Zuberi Homera amesema uwepo wa Kampuni za gesi za TOL Gases unakwenda kuongeza kasi ya uwekezaji katika Mkoa wa Mbeya.



Mheshimiwa Homera ameyasema hayo mara baada ya kupokea taarifa ya Kampuni hiyo kuhusu uwekaji wa mtambo mpya wa gesi ya carbon dioxide katika eneo la Ikama wilayani Rungwe. kutoka katika Kampuni hiyo

Akizungumza mbele ya wanahabari Ofisini kwake jijini Mbeya Homera ameitaja Kampuni ya TOL Gases kuwa inaendelea kuongeza uchumi wa Mkoa na kwamba kiwango kikubwa cha gesi hiyo kinapatikana ndani ya Mkoa wa Mbeya.

“Uwepo wa Kampuni ya TOL Gases kwenye maonesho ya nanenane kitaifa Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ndani ya viwanja cha John Mwakangale,imechagiza vizuri kuonesha uwekezaji unavyopiga kasi mkoani Mbeya’’,alisema.

Hata hivyo ametoa rai kwa kampuni ya TOL Gases na kampuni nyingine  kushiriki katika maonesho ya nanenane mwaka huu ili kuonesha uwekezaji mkubwa unaofanyika mkoani Mbeya.

 Amesisitiza kuendelea kuongezeka kwa  Kampuni kubwa mkoani Mbeya zikiwemo kampuni za kukamua mafuta ya palachichi na kampuni kubwa za  uvunaji wa gesi ya Carbon dioxide kwenye eneo la Ikama wilaya ya Rungwe ni dalili njema ya Mkoa huo kusonga mbele.

Kampuni ya TOL Gases iliyoanzishwa miaka Zaidi ya 70 inamilikiwa na watanzania wapatao 10,711 kupitia soko la Hisa la Dar es salaam na  inajihusisha na uzalishaji wa gesi za viwandani na hospitalini.

Kampuni hiyo kupitia kiwanda chake cha carbon dioxide inahudumia viwanda mbalimbali hapa nchini hivyo kuchochea ukuaji wa viwanda,hasa viwanda vya vinywaji baridi.

Kulingana na taarifa ya kampuni hiyo,pia gesi hiyo inauzwa nchi za nje kama vile Congo DRC,Zimbabwe,Zambia,Malawi na Burundi.

Kampuni ya TOL Gases Julai 29 mwaka huu inatarajia kuweka mtambo mpya wa gesi ya carbon dioxide katika eneo la Ikama wilayani Rungwe.

Mtambo huo mpya utapoanza uzalishaji utaongeza kodi za serikali(Mrabaha),kodi ya mapato, ushuru wa Halmashauri na kuongeza mauzo ya nje hivyo kuongeza fedha za kigeni.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari,Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.