TNGP KUIBUA KERO KONDOA

Na Nizar Mafita, KONDOA 

Mtandao wa jinsia TNGP waibua kero katika vijiji vilivyomo kata ya Haubi wilayani Kondoa 

 


Miongoni mwa kero zilizo ibuliwa na mtandao huo ni ukosefu wa maji, uhaba wa Ardhi kwajili ya shughuli za kilimo na kero ya Tasaf inayotolewa kwa kaya maskini

 

Kero hizo ibuliwa wilayani Kondoa katika mafunzo yanayoendelea ya ukatili wa kinjinsia yanatolewa TNGP. 

 

Akizungumza Anna Grace Rombiza amabye ni mtaalam elekezi wa masuala ya jinsia amesema wamefika taika kata ya Haubi wilayani Kondoa kwajili ya kutia elimu ya Ukatili wa kinjinsia ili jamii iweze kufahamu vyema aina zote za Ukatili wa kinjinsia na kuweza kukabiliana nazo pindi vitendo vya Ukatili vinapo tokea katika jamii 

 

"Tumekuja hapa Haubi kwaajili  kuwezesha masuala ya yote ya kijinsia lengo ni kuwezesha na kuweka mikakati ya ufumbuzi lakini pia wao wemeweza pia kuibua na kuibua kero zilizopo katika jamii yao "

 

Aidha, pia bi Grace amsema wameibua kero ya Ardhi ambayo haitoshelezi baada ya wakazi wa Kijiji cha Mafai  kutakiwa kupisha maeneo ya  pori la akiba la mkungunero na hivyo kupelekea kuwepo kwa Ukatili wa kiuchumi  baada ya kukosa maeneo ya uzalishaji na kuacha shuguli za uzalishaji mama pekee 

 

Akijibia kero zilizoibuliwa na washiriki wa wa semina Diwani wa kata ya Haubi, Paul irovya amekiri kuwepo kwa  wa kero hizo katika kata na kusema zipo katika za utatuzi na kero ya Tasaf amesema kuwepo kwa changamoto kwa msimu huu wa uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kukosa baadhi ya wombea kwa kutokuchukuwa fomu kisa watakosa sifa ya kupata msaada wa huduma za TASAF wa kaya masikini kwasababu  watakuwa viongozi wa vyama vya siasa na pia akizungumzia kero ya maji katika Kijiji cha Ntomoko chenye chanzo cha mradi mkubwa wa maji kushindwa kuwanufaisha wenyeji wa kijiji hicho cha Ntomoko na badaka yake kwenda kuwanufaisha wilaya ya jirani ya Chemba.

 

"Watu Sasa wanogopa kuchukuwa fomu za kugombea nafasi za uongozi CCM kisa watakosa  sifa ya kupata msaada wa huduma za Tasaf na ukiangalia kweli mtu anazo sifa za huduma lakini anakwamishwa kwakuwa ni kiongozi wa chama cha siasa binafi ningependekeza sheria hi ingaliwe

 

Kwa upande wa washiriki wa semina wameahidi kwenda kuwa mabalozi katika vijiji vyao katika masuala ya Ukatili wa jinsia katika jamii yao ili kurahisisha jamii kuelewa Athari za vitendo vya Ukatili wa kinjinsia.




Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.