OFISI YA WAZIRI MKUU YATOA MAFUNZO YA UJUZI TEPE KWA MAKUNDI MAALUM YA VIJANA SHINYANGA.

 



 

OWM - KVAU.

OFISI ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) imetoa mafunzo ya ujuzi tepe ‘Soft Skills’ kwa makundi maalum ya vijana katika Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga yenye lengo la kujitambua na kujithmini.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo ya siku tatu yanayofanyika kuanzia leo Jumanne Juni 28,2022 hadi Juni 30,2022 katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Julius Tweneshe amezitaja miongoni mwa mada zitakazofundishwa ni pamoja na kujitambua kama wajasiriamali, ujasiriamali na masoko.

Mada zingine ni urasimishaji wa biashara na usimamizi wa fedha, afya ya uzazi na ujinsia,afua zilizopo kwa ajili ya vijana wenye ulemavu na mama wadogo,afua zilizopo kwa ajili ya vijana wanaoishi na Virusi vya Ukimwi.

“Vijana hawa pia watapewa mafunzo kuhusu fursa za uwezeshaji wa vijana kiuchumi ngazi ya taifa na mkoa, fursa za mitaji na huduma kwa wajasiriamali zinazotolewa Wataalamu kutoka taasisi mbalimbali, stadi za uongozi, taratibu za uundwaji wa vikundi,uundwaji wa vikundi vya uzalishajimali vya vijana, kubainisha mahitaji ya vikundi na uandaaji wa andiko mradi”,ameongeza Tweneshe.

Mwisho.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.