JIJI LA DODOMA LAPONGEZWA UTEKELEZAJI MIRADI YA MAENDELEO

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa ujenzi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayolenga kusogeza huduma kwa wananchi na kuongeza mapato.

Zuberi White


Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Dodoma, Zuberi White alipokuwa akifungua Mkutano wa mwaka wa ALAT Mkoa wa Dodoma uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma mwishoni mwa wiki.

White alisema kuwa walitembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuridhishwa na utekelezaji wake. “Tumeona wenzetu wanavyotekeleza mradi wa ujenzi wa hoteli ya Dodoma City, ujenzi wa soko la wazi la Machinga, ujenzi wa Kituo cha Afya Chang’ombe, ujenzi wa shule ya mchepuo wa kiingereza, ujenzi wa shule ya sekondari Hombolo Makulu na ujenzi wa jengo la kitega uchumi Mtumba, kwa kweli wenzetu hawa wapo vizuri na wamejipanga sawasawa” alisema White.

Alisema kuwa miradi hiyo ni mizuri. Pamoja na kutoa huduma bora kwa wananchi, miradi hiyo itaongeza mapato ya halmashauri, alisema.

Mkutano wa mwaka wa ALAT Mkoa wa Dodoma ulifanyika katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ukitanguliwa na ziara ya siku moja ya kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa jijini hapo.

 

MWISHO

 


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.