Na. Dennis Gondwe, DODOMA
JUMUIYA ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa
Dodoma inajivunia kupandisha kiwango cha ufaulu katika mkoa kutoka nafasi ya 23
mwaka jana kwa elimu ya sekondari.
Zuberi White |
Kauli hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya
Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Mkoa wa Dodoma, Zuberi White alipokuwa
akifungua mkutano wa mwaka wa ALAT mkoa uliofanyika mwishoni mwa wiki katika
ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.
White alisema “ALAT Mkoa wa Dodoma tumetekeleza kwa
asilimia 90. Vikao vyetu vyote vimefanyika kwa mujibu wa ratiba. Kwa upande wa
elimu ya sekondari, Mkoa wa Dodoma tumepanda sana. Dodoma tulikuwa nafasi ya
23, ila mwaka tumepanda sana na kukosa pointi moja kuingia 10 bora. Hongera kwa
wenyeviti na wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dodoma kwa kazi nzuri”.
Mwenyekiti huyo aliwashauri wajumbe kuihamasisha jamii
ili watoto wasome. “Tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwa kutupatia fedha za
mapambano dhidi ya UVIKO-19. Mheshimiwa Rais ametusaidia sana katika
kukamilisha madarasa. Wanafunzi wote wamepelekwa shule na hatukuwa na chaguo la
pili msimu huo” alisema White.
Aidha, aliwakumbusha kuwa uchumi na maendeleo ni mambo
yanayokwenda pamoja na kuwasisitiza kuinua uchumi wa wananchi wao. “Karibuni
Dodoma makao makuu ya nchi. Niwahakikishie ni salama kwa watu wote” alisisitiza
White.
Mkutano wa mwaka wa ALAT Mkoa wa Dodoma ulifanyika
katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma ukitanguliwa na ziara ya siku moja ya
kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa jijini hapo.
MWISHO
Comments
Post a Comment