WAZIRI DKT MABULA ATAKA ‘CLINIC’ ZA ARDHI KUTATUA CHANGAMOTO ZA ARDHI

 

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza kwenye kikao chake na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa na watendaji wa Makao Makao Makuu mara baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara yake jijini Dodoma mwishoni mwa wiki.  Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Ardhi Ridhiwani Kikwete.

Na Munir Shemweta, WANMM DODDOMA

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline, Mabula amewataka Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa mikoa nchini kuanzisha Clinic za Ardhi kwa ajili ya kushughulikia changamoto za sekta ya ardhi katika mikoa yao

‘’Mjiwekee utaratibu mzuri wa kusikiliza changamoto za ardhi katika mikoa yenu kwa kuanzisha Clinc za ardhi, Mwanza wamekuwa wakifanya hivyo na wamefanikiwa’’ alisema Dkt Mabula

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, mbali na Wizara yake kufanya vizuri  kwa baadhi ya mambo lakini kuna changamoto ya kutokuwa makini kwa watendaji na kutolea  mfano wa barua za malalamiko zinazokwenda kwenye ofisi yake kuwa zingeweza kushughulikiwa katika mikoa husika.

‘’Changamoto kubwa hatuko serious, barua za malamimko ya migogoro ya ardhi zinakuja kwa waziri na mimi nazirudisha kwenu kupata ufumbuzi na huko napata majibu why msingeshughulikia mpaka zije huku? Ndiyo maana migogoro inakuwa mingi’’ alihoji Waziri Dkt Mabula.

Waziri wa Ardhi alisema hayo mwishoni mwa wiki wakati akizungumza na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa na watendaji wa Makao Makao Makuu mara baada ya kupitishwa kwa Bajeti ya Wizara yake na Bunge ambapo kiasi cha shilingi 110,323,474,000 kiliidhinishwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, sehemu kubwa ya migogoro ardhi inachangiwa na kutokuwepo mipango ya matumizi bora ya ardhi kwenye halmashauri hivyo aliwataka Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa mikoa kuzikumbusha halmashauri katika mikoa yao kutenga fedha kwa ajili ya mipango hiyo.

Aidha, aliwataka pia kuhakikisha pesa ambazo halmashauri zinazokopeshwa kwa ajili ya miradi ya kupanga, kupima na kumilikisha ardhi zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na ile faida inayopataikana itumike kuboresha sekta ya ardhi.

Kuhusu urasimishaji makazi holela, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliwataka Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa kuhakikisha makampuni yaliyoshindwa kukamilisha kazi za urasimishaji yanachukuliwa hatua na kuangalia namna bora ya kukwamua kazi zilizokwama.

‘’Kama wao wamekwama kukamilisha kazi za urasimishaji ninyi mnafanyaje? Undeni timu katika mikoa kwenda wilaya moja hadi nyingine kulingana na mahitaji, zoezi hili lina chanagamoto kubwa sana mfano mkoa wa Tabora umefanya vizuriu sana’’ alisema Dkt Mabula.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Ridhiwani Kikwete alikemea ucheleweshaji hati kwa wamiliki wa ardhi na kueleza kuwa, kama kuna tatizo linalosababisha mwananchi kutopata hati yake haraka basi aelezwe badala ya kumuacha mpaka aanze kulalamika.

‘’Kuna kilio cha wananchi hati kuchukua muda mrefu, nina mfano wa Dar es Salaam kuna mama mmoja hati yake ilichukua miaka saba na tatizo lake ilikuwa kitambulisho cha NIDA lakini hakuelezwa hadi akaja kulalamika kwangu, kama lipo tatizo mhusika aelezwe mapema, maduhuli yanakosekana kutokana na wananchi kutopewa hati’’ alisema Ridhiwani.

Dkt Allan Kijazi, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alieleza kuwa, ipo changamoto kwa baadhi ya watumishi kufanya kazi bila kufuata taratibu na taarifa zao hazitolewi na Makamishna wa Ardhi wa Mikoa husika jambo alilolieleza kuwa, linalosababisha wizara kupata taarifa kupitia vyanzo vingine,

‘’Kuna changamoto ya watendaji kufanya kazi bila kufuata taratibu na taarifa hazipatikani na pale zinapopatikana ni kutoka other sources sasa utendaji wenu utapimwa pia na jinsi unavyosimamia watendaji wako’’ alisema Dkt Allan Kijazi.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.