WAFANYABIASHARA SOKO LA MAJENGO WAHIMIZWA KUZINGATIA USAFI KATIKA MAENEO YAO YA BIASHARA

 


Na Mwandishi Wetu, Dodoma.

Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira imewataka wafanyabiashara wa Soko la Majengo jijini Dodoma kuyaweka mazingira ya kufanyia biashara katika hali ya usafi  ili wateja wanapo kwenda kununua bidhaa ikiwemo vyakula wakute mazingira ambayo ni safi na salama.

Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Marry Maganga wakati akizungumza na wafanyabishara wa soko hilo mara baada ya kufanya ziara ya kikazi kwaajili ya kujionea jitihada za wadau katika usafi wa mazingira.

‘’Mazingira ni afya kwa hiyo  mjitahidi kuyaweka katika hali ya usafi ukizingatia kwamba chakula kinauzwa  hapa . Sasa mtu anapokuja kununua bidhaa ya chakula anategemea aikute kwenye mazingira ambayo ni safi.’’ Maganga

‘’Mjitahidi kuzingatia usafi, mnajitahidi sana pamoja na mazingira kuwa madogo mnajitahidi kadiri ya uwezo wenu. Basi muongeze nguvu.'' ameongeza Maganga   

Kwa upande wa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Ramadhan Kailima amewahimiza kufanya mikutano ya kila mwezi ambayo itakuwa na ajenda ya mazingira itakayo saidia kuboresha mazingira ya usafi katika soko hilo.

‘’Tunapongeza uongozi wa soko namna ambavyo imejipanga . Na niwaombe wafanya biashara wote tuzingatie usafi bila kufanya usafi hatuwezi kufanya jambo lolote.’’ amesema Kailima

Ziara hiyo ni sehemu ya Wiki ya Mazingira ambapo kilele chake kitakuwa Juni 5,2022.

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.