RAIS SAMIA APONGEZWA KWA KUFANYA MABORESHO YA MASLAHI YA WATUMISHI

 



Dodoma.

Taasisi ya Jamii Mpya Dodoma imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kufanya maboresho ya maslahi ya watumishi kwa kupandisha kiwango cha mshahara kwa asilimia 23.

Hayo yamesemwa leo na Mratibu wa Taasisi hiyo mkoa wa Dodoma  Nurdin Ngapanya wakati akizungumza na waandishi wa habari, amesema mbali na maboresho hayo amepandisha pia kiwango cha mafao kwa mkupuo kwa wastaafu kufikia asilimia 33 kwa watumishi na sekta binafsi.

'' Maboresho haya yanakwenda kumgusa kila mtanzania na  hatimaye kuleta ustawi wa jamii.’’ amesema Ngapanya

Wakati huo huo, Ngapanya amewahimiza watanzania kote nchini kujitokeza kwa wingi kuhesabiwa katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi linalo tarajiwa kufanyika mwezi Agosti,2022.

‘’Kila familia iwe na mabalozi wa Sensa ya Watu na Makazi tuhimizane sisi kwa sisi majirani na jamii zinazo tuzunguka twendeni tushiriki kikamilifu kwenye zoezi hili.’’ amesisitiza Ngapanya

‘’Tusije tukapoteza fursa hii adhimu ambayo haitokei tena  mpaka ipite miaka 10. Sisi tumejipanga kupita kata kwa kata ,mtaa kwa mtaa nchi nzima kuhamasisha kushiriki zoezi la Sensa ya Watu na Makazi. Tunaomba pia makundi na taasisi nyingine tuungane na serikali yetu kuhamasisha zoezi la Sensa.’’ amehimiza Ngapanya

Mwisho

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.