OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YAKANUSHA ORODHA INAYOSAMBAA MITANDAONI KUHUSU KUTOKA KWA NAFASI ZA KAZI KWA MAKARANI

Na. Rhoda Simba, DODOMA

 

OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imekanusha taarifa zinazosambaa Katika mitandao ya kijamii kuhusu Kutoka kwa orodha ya majina kwa nafasi za kazi kwa makarani na wasimamizi wa sensa ya watu na makazi.

 

Dkt. Albina Chuwa

Taarifa hiyo imetolewa Leo Mei 27 jijini hapa na Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Dkt. Albina Chuwa wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema taarifa hiyo siyo rasmi kwa watanzania waliyo omba nafasi za ukarani na usimamizi wa Sensa Katika maeneo wanayoishi.

 

"Kwenye Taarifa inayofanana na hii ambayo pia sio rasmi watu hawa ambao hawana nia nzuri kwa Serikali na watanzania kwa ujumla wamekwenda mbali na kutamka tarehe ya usahili kuwa ni tarehe 29 Mei 2022, napenda ifahamike kwamba mchakato wa ajira za muda za makarani na wasimamizi wa Sensa Bado unaendelea Katika ngazi ya kata shehia na Halmshauri zote" amesema Dkt. Chuwa.

 

Amesema zoezi la uchambuzi wa maombi kwa waombaji wote linatarajiwa kuanza tarehe 02 Juni 2022 kwenye Kila kata au shehia husika baada ya kukamilika kwa mafunzo ya maafisa watakaohusika kufanya usahili.

 

"Mchakato wa ajira za makarani na wasimamizi wa sensa linakwenda vizuri kulingana na ratiba ya sensa" amesema Dkt. Chuwa.

 

Hata hivyoo Dkt. Chuwa amewataka wananchi kwamba taarifa yoyote kuhusu mwenendo wa maandalizi ya sensa ya watu na makazi sensa ya majengo na sensa ya anwani za makazi ikiwemo ajira za Muda zitatolewa na Serikali kupitia vyombo vya habari.

 

Mwisho

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.