MKURUGENZI DODOMA JIJI AMPONGEZA RAIS SAMIA KUBORESHA MASLAHI YA WATUMISHI


Na. Theresia Francis, DODOMA

MKURUGENZI wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru ampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kuboresha maslahi ya watumishi wa umma wa Tanzania na kutoa shilingi bilioni 2.5 za umaliziaji wa Soko la wazi la Machinga.

Joseph Mafuru


Pongezi hizo alizitoa leo katika hafla fupi ya kumshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuboresha maslahi ya watumishi katika ukumbi wa mikutano wa PSSSF jijini hapa.

Mkurugenzi Mafuru alisema kuwa Rais Samia toka akabidhiwe nchi ameweza kuimarisha miundombinu kwa kiasi kikubwa na kuboresha maslahi ya watumishi. Maboresho hayo yanapelekea ufanisi wa kazi kwa watumishi wa umma kuongezeka. “Baada ya Rais kutangaza ongezeko la asilimia 23.3 kwenye mishahara yao. Watumishi sasa wanafanya kazi kwa bidii, ukienda kwenye kata unawakuta, kwenye mitaa unawakuta wanasimamia miradi ya maendeleo kwa kasi kubwa. Morali ya watumishi imerudi juu” alisema Mafuru.

Mkurugenzi huyo aliwashauri watumishi kuendana na kasi ya maboresho ya maslahi ya watumishi wa umma aliyoyafanya Rais Samia Suluhu Hassan. “Kuanzia Julai, mishahara ya watumishi inaenda kubadilika, sitegemei kufika Agosti au Septemba kuona wananchi wakiendelea kupata huduma ileile kama ya miaka miwili iliyopita. Ni deni kwetu watumishi kupambana kuonesha kuna kitu kimeongezeka kwenye utekelezaji wa majukumu yetu” alisema.

Aidha, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza kiasi cha shilingi bilioni 2.5 ili kumalizia mradi wa Soko la wazi la Machinga. Alisema kuwa halmashauri yake ilitoa kiasi cha shilingi bilioni 4.9 kwa ajili ya awamu ya kwanza ya ujenzi huo.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.