DKT. JAFO: IYUMBU PARK IKITUMIKA VIZURI INAWEZA KUWA CHANZO CHA UTALII

 


 

DODOMA.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Seleman Jafo amesema eneo  la msitu la Iyumbu Park likitumika vizuri linaweza kuwa chanzo cha utalii na kuvutia watu wanao kuja Dodoma ili waweze kujionea utalii uliomo katika eneo hilo.

Eneo hilo lina zaidi ya hekari 3000 limekuwa eneo maalum lililo tengwa kwaajili ya kupanda miti.

Dkt. Jafo ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma wakati akizindua rasmi Wiki ya Mazingira , amesema katika baadhi ya miji wamekuwa wakiingiza fedha nyingi kupitia maeneo maalum  ya misitu  yaliyo hifadhiwa ambayo yamo katikati ya jiji kwa watalii wanao kwenda kutembelea maeneo hayo.

‘’Na hapa Dodoma tumetenga eneo hili. Na Dodoma ni makao Makuu ya nchi yetu . Sasa nina amini miti hii tukiipanda na kuitunza itakuwa ni jambo jema sana . Ndugu zangu kama mnavyo fahamu mabadiliko ya tabianchi yamekuwa na changamoto kubwa duniani . Hali ya leo hii mnaona suala zima la ukame maeneo mbalimbali mvua zinazo nyesha hazitoshelezi yote ni changamoto ya ukame.’’ amesema Dkt. Jafo

Kwa upande wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Antony Mtaka ameagiza kwa kila mtu mwenye kiwanja  Dodoma kuhakikisha  anapanda miti ya matunda na miti ya kuvuli ili kuandoa changamoto za utapiamlo na udumavu unao sababisha kutozingatia lishe bora.

‘’Hata ukiangalia katika maeneo mengi tuliyo pita hakuna miti ya matunda ,huoni michungwa,huoni miembe . kwa hiyo tunajaribu kuhamasisha kuwa mabalozi wazuri wa upandaji wa miti katika familia .‘’ amehimiza Mtaka

Naye, Mkurugenzi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Dkt. Andrew Komba amesema miti 441 imepandwa katika eneo hilo huku lengo likiwa ni kupanda miti 3000.

‘’ Mwaka jana tulipanda miti mahali hapa tulipanda miti takribani 241. Kazi tunayo fanya ni muendelezo wa kazi tuliyo kuwa tukiifanya na tutaendelea kuifaanya . Lengo ni kuhakisha kwamba eneo lote hili la Iyumbu Park linaenda kupandwa miti.’’

Wiki ya Mazingira imezinduliwa ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku Mazingira Duniani yanayo tarajiwa kufanyika Juni 5,2022.

Mwisho.

 

 

 


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.