DC SHEKIMWERI ASHAURI WATUMISHI KUTENDEA HAKI ONGEZEKO MISHAHARA

Na Shaban Ally, DODOMA

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri awashauri watumishi wa umma kutendea haki ongezeko la asilimia 23.3 ya mishahara yao iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya kazi kwa uadilifu na ubunifu kwa kuzingatia haki na maslahi mapana ya nchi.  

Jabir Shekimweri


Ushauri huo aliutoa leo katika hafla fupi ya kumshukuru na kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuboresha maslahi ya watumishi katika ukumbi wa mikutano wa PSSSF jijini hapa.

“Kutokana na juhudi na kazi kubwa inayoendelea kufanywa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, sisi kama watumishi wa umma tusishangilie ongezeko la mishahara bali tunapaswa kutendea haki mishahara iliyoongezwa na Mheshimiwa Rais" alisema Shekimweri.

Mkuu wa wilaya huyo alitoa rai kwa watumishi wa umma kuboresha maisha yao katika kipindi hiki cha ongezeko la mishahara. Alisema kuwa watumishi wengi wa umma wamekua wakiishi maisha ya taabu kutokana na kutokuwepo na matumizi mazuri ya mishahara yao.

Aidha, alimpongeza Rais, Samia Suluhu Hassan kwa kutunukiwa tuzo ya uendelezaji wa miundombinu na Benki ya Maendeleo ya Afrika pamoja na kuwa miongoni mwa viongozi 100 bora wenye ushawishi duniani walioorodheshwa kwenye jarida la kimataifa la Forbes.

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.