Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana ameipongeza timu ya mpira wa Miguu ya Wizara ya
Maliasili na Utalii kwa kuwa mshindi wa kwanza kwenye michezo ya Mei Mosi.
![]() |
Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Dkt. Pindi Chana (kushoto) |
Mhe. Chana licha ya kuipongeza timu hiyo amewapongeza wachezaji na
kuwataka watumie ushindi huo kama chachu ya kuongeza juhudi na ufanisi kazini
utakao endana na kasi ya matokeo chanya ya Filamu ya The Royal Tour
iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu
Hassan Jijini Arusha.
Kwa upande wake Katibu wa Michezo wa Wizara ya Maliasili na Utalii,
(Maliasili Sports Club) Bi. Labi Masalu amemshukuru Mhe. Waziri Pindi Chana kwa
kuiunga mkono Club hiyo ya michezo na akiahidi kutekeleza agizo
alilowapa.
Michezo ya Mei Mosi hufanyika kila mwaka kwa kujumuisha wafanyakazi wote
wa Serikali na Sekta binafsi ambapo kwa mwaka huu yamefanyika Jijini Dodoma na
timu ya miguu ya Wizara ya Maliasili na Utalii kuibuka na ushindi.
Comments
Post a Comment