PROFESA MKENDA ASEMA IPO HAJA YA KUPELEKA MIKOPO KWENYE ELIMU YA VYUO VYA UFUNDI.




Na Rhoda Simba, Dodoma.

WAZIRI wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof Adolf Mkenda amesema kuna umuhimu wa kuangalia upya namna bora ya kupeleka mikopo katika elimu ya ufundi angalau kwenye ngazi ya stashahada kwa vyuo vya ufundi na ujuzi.

 

Prof mkenda ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akizungumza na bodi ya mikopo (HELSB) ambapo amesema kuwa waombaji wengi hukosa mikopo wanayoomba kutokana na kutofuata maelekezo pamoja na kutoambatanisha taarifa zote zinazomhusu muombaji.

 

Amesema taaluma za ujuzi ndizo zinazohitajika kwenye ajira kwani kilio cha watu wengi ni ajira na sehemu yenye ajira zaidi ni sehemu ya ujuzi na ufundi.

"Mwaka mpya wa fedha ujao sio Mwaka huu tutapeleka fedha kwa ajili ya wanafunzi wa ufundi kuweza kupata mikopo"amesema Mkenda

 

Katika hatua nyingine amesema ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali CAG Charles Kichere aliyoitoa hivi karibuni ilieleza kuna shida katika bodi ya mikopo hasa katika zoezi zima la ugawaji wa mkopo ni kutokana na wanafunzi wenyewe kuandika taarifa zisizosahihi na wengine kuchelewa kuomba mkopo.

 

Amesema wamezungumza na bodi na wamepata taarifa kuwa tatizo lilikuwepo huko nyuma na sasa kuna maboresho makubwa mpaka sasa na juhudi za kuboresha zitaendelea .

 

"Kwa sababu mkopo unatolewa kwa taarifa zinavyotolewa na wanafunzi wanaomba mkopo hivyo mwanafunzi akichelewa au ukitoa taarifa sio kamili anaweza kukosa mkopo ingawa una vigezo vya kupata mikopo," amesema 

 

Na kuendelea"tumekubaliana na bodi ya mikopo tunaendelea kuchakata na kila mtu ambaye CAG ameona amekosa mkopo na aliyestahili kupata mkopo kuwe na taarifa itakayokwenda bungeni na kukukutana  na kamati ya bunge na hapo kutakuwa na fursa ya kuhabarisha Umma zaidi," amesema.

 

Hata hivyo amesema ukaguzi huo ulifanyika kama miaka miwili iliyopita na maboresho yamefanyika na maboresho yanaendelea ili kuhakikisha wale wote wanafunzi wanaostahili kupata mkopo waweze kupata mkopo.

 

Pia Prof. Mkenda ametoa wito kwa wanafunzi wanaomba mkopo pindi wanapoomba mikopo kuandika taarifa iliyosahihi na kusema kuwa ukikosea kitu kimoja na bila ushahidi unaweza kukosa na wanapokwama watoe taarifa kwa bodi ya mikopo na bodi imesema watajitahidi kushughulikia kwa haraka.

 

 

Aidha,prof mkenda amesema Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia imetenga bajeti kwajili ya wanafunzi wanaofanya vizuri upande wa sayansi watapata udhamini wa masomo(scholarship) huku akiyataka makapuni mbalimbali nchini kutoa fursa kwa wanafunzi ili kuwatia moyo wasome kwa bidii na kupata ufaulu mzuri.

 

Kwa upande wake Prof.Hamisi Dihenga Mwenyekiti wa bodi ya mikopo (HELSB) amesema wao kama bodi watahakikisha kwamba utaratibu wa kutoa mikopo ni utaratibu unao eleweka pamoja na kuhakikisha mikopo wanayotoa inawalenga wale wanaostahili kupewa.

 

MWISHO.

 


Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.