Na Rhoda Simba, Dodoma.
WAZIRI wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye amewataka wafanyakazi wa
Wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii na weledi kwa kuzingatia misingi ya
sheria, haki na ustawi kwa wateja wanaowahudumia.
Waziri Nape ameyasema hayo leo
Aprili 30 jijini hapa katika kikao cha wafanyakazi wa Serikali na Afya
TUGHE ambapo amesema baadhi ya watumishi wa umma wanafanya
kazi kwa mazoea hali inayoathiri uwajibikaji wa pamoja katika utoaji wa
huduma kwa wananchi.
“Ninawaomba watumishi tuache
kufanya kazi kwa mazoea, ondokeni katika kufanya kazi kwa analojia na badala
yake tuhakikishe tunafanya kazi zitakazoacha alama"amesema Nape
“Kila binadamu ana vipawa
ambavyo Mungu amempa, ni matumaini yangu kwamba haya tunayoanza kuyajenga sisi
wafanyakazi tutayatumia vizuri, tutimize wajibu wetu na kila mmoja kwenye eneo
lake aone umuhimu wa kuwa hapo alipo.”ameongeza Nape
Pamoja na hayo, amesema Wizara hiyo inasimamia
miradi mikubwa kadhaa ambayo itabadilisha na ni vizuri kama Wizara wakawa na
uelewa wa pamoja wa miradi kupitia semina mbalimbali.
“Dunia inabadilika na sisi tuko
kwenye Wizara ambayo inajenga kesho, mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanabadilisha namna ambavyo tunapaswa kufanya kazi hivyo ni muhimu kila mmoja
kwenye eneo lake kuhakikisha anafkiria zaidi ya ‘google’ ili kuonesha umuhimu
wa kuwa katika nafasi hiyo”amesema
Naye ,Katibu Mkuu Wizara ya
Habari mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt Jimmy Yonazi
ameahidi kuboresha mazingira ya kazi kwa wafanyakazi.
“Jambo la kufanya kazi kwa
furaha kwangu mimi ni kipaumbele, wajibu na nia, kila mmoja anatakiwa kufanya
kazi kwa uhuru na kuruhusiwa kufikiri kwa sababu kufikiri kwa uhuru kunaleta
ubunifu,
“Katika ulimwengu wa sasa,
uchumi wa kidijitali hauna mipaka, vivyo hivyo kwa habari, Mawasiliano na
Teknolojia ya Habari havina mipaka kwa hiyo, tunamshkuru Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuamua kuunda Wizara hii na
kuifanya nchi yetu kuwa moja ya nchi ambazo zina Wizara mahususi katika sekta
hizi.”Amesema Yonazi
Kwa upande wake muwakilishi wa TUGHE Laurencia Masigo amesisitiza umuhimu wa mafunzo kwa wafanyakazi ili kuendana na mabadiliko ya kiteknolojia.
“TUGHE inaipongeza Wizara kwa kupata hati safi kwa mwaka huu, tunawapongeza kwa sababu huo ni mchakato mrefu kuanzia kuweka mikakati na kuifuatilia, kupata fedha na kusimamia kazi mpaka kuja kukaguliwa na Wakaguzi na kupata hati safi, hili ni jambo la kujivunia,''
“TUGHE inaomba Watumishi waendelee kupatiwa mafunzo ya muda mfupi na mrefu ili kuweza kuendana na hali halisi ya mabadiliko ya kidijitali”amesema Masigo..
Mwisho.
Comments
Post a Comment