MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR MIRADI INATEKELEZWA KWA USHIRIKIANO

Na. Mwandishi Wetu,

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema utekelezaji wa miradi upande wa Zanzibar ni matunda ya ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

 

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla

Amesema hayo wakati wa hafla ya utiaji saini wa makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba kwa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi ambapo mradi huo utatekelezwa na Kampuni ya Dezo Civil Contractors Co. Limited.

 

Mhe. Hemed alisema kuwa SMZ inafarijika kuona mradi huo unaanza kutekelezwa kwa vitendo na kwamba utaleta manufaa makubwa kwa wananchi watakaonufaika na mradi huo.

 

Pia alitoa pongezi na shukrani kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango pamoja na Ofisi yake kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa SMZ.

 

Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeonesha dhamira yake ya kusaidia kumaliza tatizo la Mazingira.

 

Awali Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Hassan Mitawi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Bi. Mary Maganga, alisema chimbuko la ujenzi wa eneo hilo ni kupitia ziara ya aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu aliyoifanya mwaka 2019 ambapo aliahidi kusimamia ujenzi wa eneo hilo.

 

Amesema tathmini katika ufukwe wa Sipwese ilionesha kuwa maji ya bahari yameingia katika maeneo ya kilimo cha mpunga na wananchi wa Shehia ya Mkungu, Kijiji cha Sipwese eneo la kwa Mgogo.

 

Mitawi alisema kujaa kwa maji haya pia yamesababisha kukatika kwa mawasiliano kutoka upande wa pili takribani kilometa 3.360 ambako ndiko wananchi wanafuata huduma za jamii kama vile shule hali inayosababisha watoto wa shule kuvuka maji shingoni kuweza kuifikia shule.  

 

“Mmomonyoko wa fukwe zilizo katika Bahari ya Hindi kwa upande wa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani umeendelea kuwa ni changamoto katika maeneo mengi ya fukwe na umeanza kuleta athari katika baadhi ya maeneo kwa kusababisha uharibifu wa miundombinu iliyopo kama vile barabara, majengo, makazi ya watu na madaraja.

 

“Hali hii imesababisha Serikali kutumia fedha nyingi katika kukarabati miundombinu iliyoharibiwa, Fedha ambayo ingeweza kupelekwa katika maeneo mengine muhimu kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijami,” alisema Mitawi.

 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Bw. Thabit Idarous Faina alisema ujenzi wa eneo hilo utasaidia changamoto inayowakabili wananchi wa eneo la Sipwese ikiwemo kuvuka kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyengine, maji ya chumvi kuingia katika eneo la kilimo pamoja na kupungua kwa eneo la makazi ya wananchi.

 

👆🏿nimefanya editing kidogoMakamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amesema utekelezaji wa miradi upande wa Zanzibar ni matunda ya ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ).

 

Amesema hayo wakati wa hafla ya utiaji saini wa makabidhiano ya eneo la mradi kwa ufukwe wa Sipwese, Pemba kwa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar iliyofanyika katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi ambapo mradi huo utatekelezwa na Kampuni ya Dezo Civil Contractors Co. Limited.

 

Mhe. Hemed alisema kuwa SMZ inafarijika kuona mradi huo unaanza kutekelezwa kwa vitendo na kwamba utaleta manufaa makubwa kwa wananchi watakaonufaika na mradi huo.

 

Pia alitoa pongezi na shukrani kwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango pamoja na Ofisi yake kwa kutoa ushirikiano mkubwa kwa SMZ.

 

Amesema Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeonesha dhamira yake ya kusaidia kumaliza tatizo la Mazingira.

 

Awali Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw. Abdallah Hassan Mitawi ambaye alimwakilisha Katibu Mkuu Bi. Mary Maganga, alisema chimbuko la ujenzi wa eneo hilo ni kupitia ziara ya aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mussa Azzan Zungu aliyoifanya mwaka 2019 ambapo aliahidi kusimamia ujenzi wa eneo hilo.

 

Amesema tathmini katika ufukwe wa Sipwese ilionesha kuwa maji ya bahari yameingia katika maeneo ya kilimo cha mpunga na wananchi wa Shehia ya Mkungu, Kijiji cha Sipwese eneo la kwa Mgogo.

 

Mitawi alisema kujaa kwa maji haya pia yamesababisha kukatika kwa mawasiliano kutoka upande wa pili takribani kilometa 3.360 ambako ndiko wananchi wanafuata huduma za jamii kama vile shule hali inayosababisha watoto wa shule kuvuka maji shingoni kuweza kuifikia shule.  

 

“Mmomonyoko wa fukwe zilizo katika Bahari ya Hindi kwa upande wa Tanzania Bara na Tanzania Visiwani umeendelea kuwa ni changamoto katika maeneo mengi ya fukwe na umeanza kuleta athari katika baadhi ya maeneo kwa kusababisha uharibifu wa miundombinu iliyopo kama vile barabara, majengo, makazi ya watu na madaraja.

 

“Hali hii imesababisha Serikali kutumia fedha nyingi katika kukarabati miundombinu iliyoharibiwa, Fedha ambayo ingeweza kupelekwa katika maeneo mengine muhimu kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijami,” alisema Mitawi.

 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Afisi ya Makamu wa Pili wa Rais Bw. Thabit Idarous Faina alisema ujenzi wa eneo hilo utasaidia changamoto inayowakabili wananchi wa eneo la Sipwese ikiwemo kuvuka kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyengine,  maji ya chumvi kuingia katika eneo la kilimo pamoja na kupungua kwa eneo la makazi ya wananchi.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.