KEISHA AMEKABITHI VYAKULA KWA WATU WENYE ULEMAVU VYENYE THAMANI YA MILIONI MOJA NA LAKI TANO

 

Na. Kadala Komba Dodoma 


Mbunge wa Viti Maalumu Khadija Shaaban Taya maarufu kama Keisha kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Wametembelea shule ya watu wenye ulemavu ya  msingi Hombolo Bwawani jijini Dodoma na kutoa msaada wa vyakula vyenye thamani ya milioni moja na laki tano.

Mbunge wa Viti Maalumu Khadija Shaaban Taya akikabidhi zawadi


Keisha Akizungumza ngumza hayo alipotembelea shule hiyo   na kujioneya mazingira wanayohishi watu wenye ulemavu, Alisema ni furaha kubwa Sana Mimi kuwepo hapa katika kipindi hiki cha mwezi mtukufu wa Ramadhani, kwa kutambua hili tumekuja kuwaona nataka mtambue kuwa Serikali anawakumbuka na kuwathamini tumekuja na hivi vitu hili kuonesha kwamba tupo pamoja.

 

Pia Keisha Alisema kazi ya mbunge ni kupaza sauti ya Changamoto ambazo wananchi wanakumbana nazo,Lengo la sisi kuja hapa ni kujua Changamoto mnazopitia mazingira mnayohishi na hivyo vyote tumekwisha viona tutavifanyia kazi. Mimi ni kama nyinyi nimesoma Kama nyinyi zingatieni masomo mtafika mbali.

 

Aidha Keisha alitumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali ya hawamu ya sita chini ya Rais Samia kwa kusikia kilio Cha watu wenye ulemavu wa Ngozi na kutenga Bajeti ya mafuta ya Ngozi kwa watu wenye Ualbino Alisema ninafuraha kuona Sasa tumepata mafuta ambayo yatatuweka salama,tumepata mafuta  Amini na kofia pia zinakuja.

 

Kwa upande wake Prof. Jamal Adam Katundu

Katibu Mkuu Ofisi ya Wziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Ametoa maagizo kwa Mkurugenzi kitengo Cha watu wenye Ulemavu Rasheed  Maftah , kuwapa kipaombele Cha Ajira walimu wanaojitolea katika   shule ya watu wenye ulemavu ya  msingi Hombolo Bwawani.

Alisema Chukua idadi ya walimu wanaojitolea kufundisha  katika shule hii wenye sifa, hili wapewe kipaombele kwenye Ajira pindi nafasi za Ajira zitakapotoka wao wapewe kipaombele .

 

Pia Katibu Alisema hawa watu wameonesha Moyo wa uzalendo na utayari wa kufanya kazi tusiwaache tuwape Ajira hili nao waone thamani ya kile wanachokifanya .

 

Sambamba na Hilo Mkuu  msaidizi wa shule hiyo Bw.Musa Simoni amemshukuru Mbunge Keisha pamoja na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa zawadi ambazo wametoa kwajili ya watoto wetu  wenye ulemavu,sisi Kama Walimu kazi yetu ni kuhakikisha hivi vitu vinawafikia walengwa, hawahaidi hivi vitu vyote ambavyo vimeletwa ikiwemo Fedha kutoka kwa Ofisi ya Waziri Mkuu imefika na itawafikia watoto waliolegwa.

 

Aidha Bw.Musa Alisema katibu wetu Mkuu ni msikivu tunamwomba asituache kwani Changamoto ni nyingi katika shule hii, mazingira ya shule sio rafiki kwa watu wenye mahitaji Muhimu Kama hawa na wewe ni shahidi umejionea Bweni wanarolala watoto wetu  tunaomba mtusaidie.

        

             MWISHO

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.