Na. Lusajo Mwakabuku, OWM-KVAU Dodoma.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira,
Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce L. Ndalichako amewataka
wajumbe wa mkutano wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika
(SADC) kuhakikisha katika mwongozo wa kulinda na kuzuia ajira mbaya kwa watoto
ni vyema maneno yaliyotumika yakapatiwa tafsiri ili yaendane na maadili,
utamaduni, na mazingira ya kiafrika.
![]() |
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce L. Ndalichako |
Waziri Ndalichako alitoa
kauli hiyo mapema leo 30/03/2022 jijini Lilongwe Malawi alipokuwa akishiriki
Mkutano wa Mawaziri wa Kazi na Ajira wa SADC waliokutana kujadili mambo
mbalimbali juu ya sekta ya Kazi na Ajira ambapo katika kikao hicho ajenda 13
zinazohusu kuweka miongozo mbalimbali ya kusimamia masuala ya ukuzaji wa fursa
za ajira, usimamizi wa viwango vya kazi, hifadhi ya jamii na usalama na afya
mahala pa kazi.
Akitoa mchango wake,
Profesa Ndalichako alisema suala la biashara ya ngono kwa mila na desturi ya
nchi zetu za Afrika ni suala lisilokubalika, hivyo alisisitiza katika mwongozo
huo isitafsiriwe kuwa biashara hiyo inakubalika kwa wasio watoto peke yake
kwani kwa mazingira na tamaduni zetu za kiafrika biashara hiyo ni haramu.
Masuala mengine
yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni pamoja na kupitia rasimu ya Itifaki ya
SADC ya Kazi na Ajira, Mwongozo wa kuanzisha Taasisi za Majadiliano ya Waajiri
na Waajiriwa, Zana za Ufuatiliaji na Utoaji taarifa kuhusu utekelezaji wa Mpango
wa Uhamaji Nguvukazi ndani ya SADC pamoja na kuanzisha mfumo wa taarifa za soko
la ajira wa SADC.
Pia mijadala mingine
ilifanyika juu ya Hali ya Utekelezaji na Uridhiaji wa Itifaki na Mikataba ya
Shirika la Kazi Duniani na pia mkutano huu ulipokea taarifa kuhusu maandalizi
ya ushiriki wa nchi za SADC katika Mkutano Mkuu wa Shirika la Kazi Duniani
(ILO) unaotaratijwa kufanyika Mwezi Juni, 2022.
MWISHO
Comments
Post a Comment