WAZIRI JAFO APONGEZA WAFANYAKAZI OFISI YA MAKAMU WA RAIS KWA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU YAO NA UTATUZI WA HOJA 11 ZA MUUNGANO

 


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) amewapongeza wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa utekelezaji wa majukumu yao ikiwemo utatuzi wa hoja 11 za Muungano ndani ya kipindi cha mwaka mmoja.

 

Ametoa pongezi hizo wakati akifungua Kikao cha Baraza la Wafanyakazi, Ofisi ya Makamu wa Rais cha kupitisha Bajeji ya Utekelezaji wa Mapato na Matumizi kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kilichofanyika leo Machi, 2022 jijini Dodoma

 

Akizungumza na wafanyakazi hao Dkt. Jafo aliwataka kuendeleza juhudi hizo ili wananchi wapate uelewa zaidi kuhusu umuhimu wa Muungano na masuala ya Mazingira.

 

Pia, Dkt. Jafo alitoa pongezi kwa wafanyakazi wa Ofisi hiyo kwa kuwajibika ipasavyo katika sekta ya mazingira ikiwemo kusimamia kampeni mbalimbali zikiwemo ‘Soma na Mti’ ambayo inahusisha wanafunzi ngazi ya shule za msingi hadi vyuo kupanda miti na hivyo kuifanya nchi yetu kuwa ya kijani.

 

“Kikubwa zaidi niwape moyo watumishi mmefanya kazi nzuri sana, sasa twendeni na spirit (moyo) tuendeleze upendo tulio nao maana bila upendo hakutakuwa na mafanikio,” alisisitiza Jafo.

 

Waziri huyo alisema vikao vya Baraza la Wafanyakazi ni muhimu katika kujadili masuala mbalimbali ya wafanyakazi kwa upana kwa kuzingatia haki, weledi ikiwa ni pamoja na kujadiliana changamoto za kiutendaji na hatua za kukabiliana nazo.

 

Aliongeza kuwa vikao hivyo vinalenga kudumisha utamaduni wa kufanya kazi kwa pamoja, bidii na maarifa ili kuleta ufanisi katika kutekeleza majukumu ya Ofisi na Taifa kwa ujumla.

 

Hivyo aliwataka wafanyakazi kujadili suala la Bajeti kwa kina na ikiwa zipo changamoto zilizobainishwa mwaka wa fedha uliopita zijadiliwe ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi ili kurahisisha Utekelezaji wa Bajeti ya Mwaka wa fedha ujao.

 

“Ninaamini Bajeti hii imejikita katika kuwezesha, kudumisha Muungano wetu na imezingiatia masuala ya uhifadhi wa mazingira yetu unaosimiwa na Ofisi hii na pia niwaombe wajumbe boresheni utendaji kazi ili Ofisi hii iwe mfano wa Taasisi na Wizara zote katika utekelezaji wa majukumu yetu kwa kuzingatia umuhimu wa Ofisi hii,” alisisitiza Jafo.

 

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.