WAZIRI DKT. NDUMBARO ATETA NA BALOZI WA MAREKANI NCHINI, DKT. DONALD WRIGHT KUHUSU UWEKEZAJI MAHIRI KATIKA MAENEO YA WANYAMAPORI (SWICA)

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Damas Ndumbaro leo amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Donald Wright kuhusu masuala mbalimbali ya Uwekezaji Mahiri katika Vitalu vya Uwindaji wa Wanyamapori 

 



Katika mazungumzo hayo Waziri, Dkt. Ndumbaro amemueleza Balozi huyo kuwa Tanzania itaendelea kuweka mazingira rafiki ya Uwekezaji kwa Wawekezaji wa kutoka Marekani hususani katika sekta ya Uwindaji wa Kitalii kwa kuzingatia maslahi ya nchi. 

 

"Moja ya shabaha yetu kama Wizara ni kuwavutia Wawekezaji, tunafanya kila liwezekanalo ili kuhakikisha Wawekezaji wa kutoka nchi mbalimbali wakiwemo wa Marekani wanawekeza katika uwekezaji huu wa muda mrefu'' amesisitiza Dkt. Ndumbaro

 

Wizara ya Maliasili na Utalii inatarajia kukusanya Sh23 bilioni kwa mwaka kutokana na uwekezaji mahiri unaoendekea kufanywa kwenye sekta ya utalii nchini

 

 

MWISHO

Comments

Dodoma News
Mwanza City, Mwanza, Tanzania
Dennis G. Harrison, mmiliki mwenza wa Mtandao wa Dodoma News Blog, alizaliwa mkoani Morogoro zaidi ya miaka 40 iliyopita. Dennis ana Taaluma ya Uandishi wa Habari (Proffessional Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine (SAUT). Mwaka 2009 alimaliza Shahada ya Uzamili katika Mawasiliano ya Umma, ikijikita katika Menejimenti ya Uhusiano kwa Umma na Matangazo katika chuo cha SAUT. Mwaka 2002, Dennis aliajiriwa katika Shirika la Posta Tanzania, Ofisi kuu ya Mwanza. Mwaka 2009 aliajiriwa katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa kwa nafasi ya Afisa Habari. Akiwa katika ofisi hiyo alifanya kazi kwa juhudu na maarifa na kufanikiwa kuchaguliwa na wafanyakazi wote kuwa mfanya kazi bora. Kufuatia juhudi na utendaji kazi wake, alipanda hadi nafasi ya Afisa Habari Mwandamizi.